728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, December 05, 2015

    RWANDA,UGANDA NANI KUTWAA TAJI LA CECAFA LEO?FAHAMU REKODI ZOTE MUHIMU

    Addis Ababa,Ethiopia.

    Timu za taifa za Rwanda na Uganda jumamosi ya leo zinatarajiwa kushuka katika dimba la Addis Ababa nchini Ethiopia katika mchezo wa fainali ya 38 wa kuwania ubingwa CECAFA Chalenji Cup.

    Mchezo huo utakaochezwa mishale ya saa 10:00 jioni kwa saa za Tanzania unatarajiwa kuwa wa vuta nikuvute kwani mshindi wa mchezo wa leo atapata kikombe na zawadi ya dola elfu 30,000.

    Uganda inaingia katika mchezo wa leo ikiringia rekodi yake nzuri mbele ya Rwanda.Uganda na Rwanda zimekutana mara 29,Uganda imeshinda michezo 15,Rwanda 8 na kutoka sare mara 6.

    Kabla ya mchezo wa fainali pia kutakuwa na mchezo wa kumpata mshindi wa tatu na wa nne ambapo wenyeji Ethiopia watavaana na Sudan saa 8:00 mchana.

    Timu ziliyotwaa ubingwa mara nyingi zaidi.

    Uganda ndiyo timu inayoongoza kwa kutwaa taji la CECAFA mara nyingi zaidi,mpaka sasa imetwaa mara 13,ikifuatiwa na Kenya iliyotwaa mara 6.

    Mabingwa wa michuano hiyo kuanzia mwaka 1999.

    1999: Rwanda B
    2000: Uganda
    2001: Ethiopia
    2002: Kenya
    2003: Uganda
    2004: Ethiopia
    2005: Ethiopia
    2006: Sudan
    2007: Sudan
    2008: Uganda
    2009: Uganda
    2010: Tanzania
    2011: Uganda
    2012: Uganda
    2013: Kenya
    2015: ???
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: RWANDA,UGANDA NANI KUTWAA TAJI LA CECAFA LEO?FAHAMU REKODI ZOTE MUHIMU Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top