728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, December 21, 2015

    RAIS:SHABIKI ALIYEMTEMEA MATE MESSI NI MPUMBAVU


    Tokyo,Japan.

    RAIS wa klabu ya River Plate Rodolfo D'Onofrio amelaani vikali vitendo vya kihuni vilivyofanywa na mashabiki wa klabu hiyo kwa nyota wa FC Barcelona Lionel Messi siku ya jumapili.

    Hatua hiyo ya D'Onofrio imekuja baada ya ripoti kudai kuwa Messi akiwa katika uwanja wa ndege wa Narita (Tokyo) alitukanwa na kisha kutemewa mate na mashabiki wa River Plate waliochukizwa na kitendo cha klabu yao kukung'utwa mabao 3-0 na FC Barcelona katika mchezo wa fainali wa kombe la dunia la vilabu ambao Messi alifunga bao la kwanza.

    Akiongea na Fox Sports D'Onofrio amesema "Ni upumbavu.Shabikia aliyefanya kitendo kile ni mpumbavu kupindukia.Nimesoma kuwa Messi amepata wakati mgumu toka kwa mashabiki wetu.

    Messi ni nembo ya soka la Argentina hata alipofunga bao la kuongoza alinyanyua mikono yake juu na kutuomba msamaha na hata baada ya mchezo alinifata na kunipongeza kwa hatua tuliyofikia hata akafikia hatua ya kuniambia kuwa enzi za utoto wake alitamani kuchezea klabu yetu"Alimaliza D'Onofrio.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: RAIS:SHABIKI ALIYEMTEMEA MATE MESSI NI MPUMBAVU Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top