728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, December 22, 2015

    ARSENAL YAICHAPA MAN CITY 2-1 EMIRATES


    London,England.

    Arsenal imeendeleza ubabe wake kwa Manchester City baada ya usiku wa leo jumatatu kuitandika kwa mabao 2-1 katika mchezo mkali wa ligi kuu England uliopigwa katika uwanja wa Emirates.

    Mabao yaliyoipa ushindi Arsenal leo hii yamepatikana kipindi cha kwanza dakika za 33 na 45 kupitia kwa Theo Walcott na Olivier Giroud wakimalizia kazi mzuri ya kiungo Mesut Ozil.

    Bao la Manchester City limefungwa na kiungo Yaya Toure kwa shuti kali dakika ya 82 akiunganisha vyema pasi ya mlinzi Bakari Sagna.

    Kufuatia ushindi huo Arsenal imeendelea kubaki katika nafasi ya pili baada ya kufanikiwa kujikusanyia pointi 36 zikiwa ni pointi 2 nyuma ya vinara Leceister City wenye pointi 38 huku Manchester City wakibaki katika nafasi ya tatu na pointi zao 32.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: ARSENAL YAICHAPA MAN CITY 2-1 EMIRATES Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top