728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, December 15, 2015

    CHELSEA YAIREJESHA LECEISTER CITY LIGI KUU,YAKUBALI KIPIGO CHA BAO 2-1 KING POWER

    Leceister,England.

    Leceister City imerejea kileleni mwa ligi kuu nchini England baada ya usiku wa leo kuibamiza Chelsea kwa mabao 2-1 katika mchezo mkali uliopigwa katika dimba la King Power,Leceister.

    Leicester City imepata mabao yake kupitia kwa mshambuliaji wake hatariJamie Vardy aliyefunga dakika ya 34 akiunganisha krosi safi ya Riyad Mahrez.

    Bao la pili la Leicester City limefungwa dakika ya 48 na Riyad Mahrez baada ya kumzidi ujanja mlinzi wa kulia wa Chelsea Cesar Azipilicueta aliyekuwa akicheza mchezo wake wa 100 na kumtungua mlinda mlango Thibaut Courtois.

    Bao la kufutia machozi la Chelsea limefungwa dakika ya 77 na mshambuliaji Mfaransa Loic Remy aliyeunganisha krosi ya Pedro Rodriguez.

    Kufuatia matokeo hayo Leicester City imefanikiwa kurejea kileleni baada ya kufikisha pointi 35 ikiishuka Arsenal yenye pointi 32 huku Chelsea ikibaki na pointi zake 14 katika nafasi ya 16,pointi 1 juu ya mstari wa kushuka daraja.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: CHELSEA YAIREJESHA LECEISTER CITY LIGI KUU,YAKUBALI KIPIGO CHA BAO 2-1 KING POWER Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top