728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, December 28, 2015

    MESSI AMTAMBIA TENA RONALDO ATWAA TUZO YA MCHEZAJI BORA WA MWAKA WA DUNIA WA GLOBE SOCCER AWARDS


    Dubai.

    Lionel Messi na FC Barcelona jana jumapili waliibuka vifua mbele baada ya kutwaa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka na klabu bora ya mwaka katika tuzo za Globe Soccer Awards 2015 huko Dubai.

    Messi aliibuka mshindi baada ya kumshinda mshindi wa mwaka jana wa tuzo hiyo Cristiano Ronaldo wa Real Madrid na Gianluigi Buffon wa Juventus.

    Mgawanyo wa tuzo ulikuwa kama ifuatavyo....

    Klabu bora ya mwaka:FC Barcelona

    Rais bora wa klabu:Josep Maria Bartomeu (FC Barcelona)

    Tuzo ya kocha bora wa mwaka imeenda kwa kocha wa timu ya taifa Ubelgiji Marc Wilmots akiwabwaga Luis
    Enrique wa FC Barcelona na Antonio Conte wa Juventus.

    Tuzo ya heshima:Andrea Pirlo na Frank Lampard 

    Wakala bora wa mwaka :Jorge Mendes 

    Tuzo ya Akademi bora:Benfica 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MESSI AMTAMBIA TENA RONALDO ATWAA TUZO YA MCHEZAJI BORA WA MWAKA WA DUNIA WA GLOBE SOCCER AWARDS Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top