728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, December 25, 2015

    MKHITARYAN MCHEZAJI BORA ARMENIA KWA MARA YA TANO MFULULIZO

    ARMENIA

    Kiungo wa Borussia Dortmund Henrikh
    Mkhitaryan ametangazwa mshindi wa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa Armenia kwa mara ya tano mfululizo huku jumla ikiwa ni mara yake ya sita.

    Mkhitaryan,ambaye amefunga magoli sita mpaka sasa na kupika mengine 11 katika michezo 16 ya ligi ya Bundesliga alitwaa tuzo hiyo kwa mara ya kwanza mwaka 2009.

    Mshindi wa tuzo hiyo hupatikana kwa kupigiwa kura na wanachama wa chama cha soka cha Armenia,Makocha,Manahodha wa vilabu na Marais wa vilabu vya ligi kuu ya Armenia,Waandishi wa habari na Wawakilishi wa vyombo vya habari.




    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MKHITARYAN MCHEZAJI BORA ARMENIA KWA MARA YA TANO MFULULIZO Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top