728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, December 16, 2015

    LIGI KUU BARA:YANGA KUIAGA TANGA LEO KWA KUVAANA NA AFRICAN SPORTS

    Tanga,Tanzania.

    LIGI Kuu ya Vodacom Tanzania Bara inatarajiwa kuendelea tena leo kwa mchezo mmoja pekee,ambapo mabingwa watetezi,Yanga SC watashuka katika dimba la Mkwakwani mkoani Tanga kuvaana na wenyeji wao African Sports .

    Mchezo wa leo ni wa pili kwa Yanga kucheza mkoani Tanga baada ya wikendi iliyopita kulazimishwa sare ya bila kufungana na Coastal Union.

    Ikiwa Yanga itapata ushindi dhidi ya African Sports leo itakuwa imefikisha pointi 27 na kukaa kileleni mwa ligi kuu ikiishusha Azam FC yenye pointi 26.

    Ligi hiyo itaendelea tena Desemba 19,2015 kwa michezo sita kupigwa

    Ndanda FC vs JKT Ruvu
    Yanga SC vs Mbeya City
    Majimaji vs Prisons
    Mwadui FC vs Simba SC
    Mtibwa Sugar vs Mgambo JKT
    Coastal Union vs Stand United


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: LIGI KUU BARA:YANGA KUIAGA TANGA LEO KWA KUVAANA NA AFRICAN SPORTS Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top