728x90 AdSpace

  • Latest News

      Wednesday, December 16, 2015

      LIGI KUU BARA:YANGA KUIAGA TANGA LEO KWA KUVAANA NA AFRICAN SPORTS

      Tanga,Tanzania.

      LIGI Kuu ya Vodacom Tanzania Bara inatarajiwa kuendelea tena leo kwa mchezo mmoja pekee,ambapo mabingwa watetezi,Yanga SC watashuka katika dimba la Mkwakwani mkoani Tanga kuvaana na wenyeji wao African Sports .

      Mchezo wa leo ni wa pili kwa Yanga kucheza mkoani Tanga baada ya wikendi iliyopita kulazimishwa sare ya bila kufungana na Coastal Union.

      Ikiwa Yanga itapata ushindi dhidi ya African Sports leo itakuwa imefikisha pointi 27 na kukaa kileleni mwa ligi kuu ikiishusha Azam FC yenye pointi 26.

      Ligi hiyo itaendelea tena Desemba 19,2015 kwa michezo sita kupigwa

      Ndanda FC vs JKT Ruvu
      Yanga SC vs Mbeya City
      Majimaji vs Prisons
      Mwadui FC vs Simba SC
      Mtibwa Sugar vs Mgambo JKT
      Coastal Union vs Stand United


      • Blogger Comments
      • Facebook Comments

      0 comments:

      Post a Comment

      Item Reviewed: LIGI KUU BARA:YANGA KUIAGA TANGA LEO KWA KUVAANA NA AFRICAN SPORTS Rating: 5 Reviewed By: Unknown