728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, September 16, 2014

    ARSENAL MBIONI KUTOA AJIRA KWA MAVETERANI



    Baada ya klabu ya Arsenal kukumbwa na balaa la majeruhi katika kikosi chake na kuwapoteza walinzi Mathieu Debuchy  na Nacho Monreal huku kukiwa na hatihati pia ya kukosa huduma ya mlinzi wake kinda Calum Chambers katika mchezo wa leo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Dortmund kutokana na kuwa majeruhi kuna jipya limeibuka klabuni hapo.
     
    Usajili umefungwa wiki mbili zilizopita,Arsenal imebaki na walinzi watatu pekee wa kujaza nafasi nne za safu hiyo.Je,unajua kinachotaka kufanyika?

    Habari zisizo rasmi sana zinasema klabu ya Arsenal imeanza mawindo ya kuhakikisha inafanya usajili wa muda mfupi (miezi 3) ili kuziba pengo lililopo katika nafasi ya ulinzi hasa kulia.Baadhi ya majina yanayotajwa tajwa ni haya yafuatayo.

    1.    Antony Reveillere (34)
    Huyo ni mlinzi wa zamani wa vilabu vya Lyon,Rennes.Aliichezea Ufaransa katika fainali za kombe la dunia mwaka 2010 pamoja na Euro 2012.

    2.     George McCartney (33)
    Nyota wa zamani wa vilabu vya Sunderland na Westham.Alitemwa na Westham msimu uliopita baada ya kuichezea klabu hiyo michezo 20.Mmoja kati ya walinzi wazoefu wa Epl.

    3.     Oguchi Onyewu (32)
    Nyota wa zamani wa vilabu vya Metz,Ac Milan,Newcastle,Qpr na Shelfield Wednesday 

                   
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: ARSENAL MBIONI KUTOA AJIRA KWA MAVETERANI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top