728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, September 12, 2014

    VALDANO:MOURINHO SI CHOCHOTE KWA GUARDIOLA



    Aliyekuwa mkurugenzi wa klabu wa klabu ya Real Madrid na mshindi wa kombe la dunia la mwaka 1986 na timu ya taifa ya Argentina Jorge Valdano amesema kocha Jose Mourinho hayuko daraja moja na kocha wa Bayern Munich Muhispania Pep Guardiola.


    Valdano aliyeichezea Real Madrid miaka ya themanini na kubahatika kuifundisha miamba hiyo kwa miaka miwili alifukuzwa katika nafasi yake ya ukurugenzi mwaka 2011baada ya kushindwa kuelewana na Jose Mourinho ambaye wakati huo alikuwa akiifundisha klabu hiyo.


    Akiongea katika uzinduzi wa kitabu chake kiitwacho “The 11 Powers of a League” Valdano alisema “Kama Guardiola ni Mozart,Mourinho ni Antonio Salieri (Mtunzi mahiri wa muziki toka Italia) ambaye angeweza kuwa mwanamuziki mkubwa kama Mozart asingekuwepo duniani”


    Valdona aliongeza “Wakati Guardiola akitwaa vikombe viwili vya ligi ya mabingwa ndani ya miaka mitatu na klabu ya Barcelona,Mourinho alishindwa kuifikisha Real Madrid japo nusu fainali katika kipindi chote alichokuwa hapo kama kocha licha ya kuwa na moja kati ya kikosi  bora zaidi katika historia ya klabu hiyo.Mara zote alikuwa akitolewa mapema katika michuano hiyo.Hiyo ni changamoto kubwa aliyoshindwa kuishinda”.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: VALDANO:MOURINHO SI CHOCHOTE KWA GUARDIOLA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top