728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, September 02, 2014

    MWANAFUNZI SHUJAA HAOGOPI KUPIGA CHABO

    ALLEN KAIJAGE aka  Middle ya juu
    0655106767
             
                                        
    Mambo mengi na ya ajabu yanaendelea kutokea Duniani.Kati ya mambo yote hayo  hakuna jambo jipya.Kinachofanyika kwenye dunia ya sasa ni muendelezo ya yaliyofanyika awali.teknolojia mpya zinafanya mambo yaonekane mapya wakati yameshafanyika.Asikudanganye mtu kuwa yeye ni mgunduzi,Wagunduzi wote walishagundua zamani na kutuachia ugunduzi wao kwenye makaratasi.Wakina newton na faraday ndio wagunduzi ila kizazi cha leo ni wabunifu kutoka kwenye kile walichokigundua wakina newton.
                 Kwenye ubunifu ndipo kuna vita ya fikira.Ndipo kwenye msuguano wa akili na ushindani wa maarifa.Ili uwe mbunifu lazima uwe na maarifa kutokana na kusoma,kusikia au kuona.unaweza ukasoma,ukasikia na kuona ila usielewe nini umesoma,kusikia au kuona.Hapa ndipo inabidi ushirikishe ubongo wako kutafakari kile ulichosoma kuona au kusikia.
                Kufikiri ndiko kunaleta matabaka,Ukiona mtu amekuzidi maendeleo ujue amekuzidi kufikiri.Mnaweza kuwa na akili sawa mkasoma kitabu au shule moja baada ya kumaliza kusoma  mwenzako akafanya mambo makubwa na wewe ukawa na maendeleo ya mwendo wa jongoo au usiwe na maendeleo kabisa hapo ujue kabisa mwenzako alisoma na kuelewa na kuanza kufikiri jinsi atakovyobadilisha nadharia kuwa vitendo,ila wewe tutakuita masikini wa fikra maana ulisoma ukamaliza bila kuelewa na kutafakari ulichosoma.
                 Watanzania tumekua na macho lakini hatuoni,tuna masikio lakini hatusikii pia tunasoma ilihali atuelewi.Kila siku tumekuwa watu wa majonzi na soka letu.Leo tukipiga hatua moja mbele kesho tutarudi hatua tatu nyuma.Kila siku tumekuwa  tukitafuta ni nani mchawi wa soka letu huku tukisahau kuwa tumejiloga wenyewe kwa kupiga kufuli bongo zetu.Viongozi wetu kabla ya kuingia madarakani huwa na mawazo mazuri sana ila ghafla akili zao uingia doa pale tu wanapopewa dhamana  ya kuongoza soka letu.
                 Kuna vitu unaweza ukafanikisha kwa njia za mkato ila sio soka.Tff wanalazimisha shubili kuwa asali.Wanamawazo na fikra nyepesi katika mambo mazito.Tangu uongozi mpya umeingia madarakani wamekuwa wakibuni mambo mengi sana wakihisi kuwa mwarobaini wa timu ya taifa na soka letu kwa ujumla,Lakini hakuna hata moja lililosaidia kati ya hayo mengi.Wamekua wakipoteza muda mwingi kuwaza juu ya maono mapya ya stars  bila kupata jawabu wakati majawabu wanayaona,ni swala la kupiga chabo nchi jirani na kuhamisha majibu kwenye makabrasha yao kwa faida ya nchi.
                   Kuna vitu vingine vya kawaida sana kufanya,hauhitaji kua na akili za newton ili kujua nini waliofanikiwa walifanya mpaka kufikia mafanikio yao.Tff wana mifano mingi wa nchi jirani zilizofanikiwa kwenye soka.Kwanini tff wanashindwa kujifunza kutoka kwenye mifano hiyo? Nchi kama Angola ni nchi ndogo kulinganisha na Tanzania tena nchi masikini ukilinganisha na nchi yetu,Lakini Angola wamefanikiwa kisoka kuliko Tanzania,Kwanini tusijifunze kutoka kwa angola.Nchi ndogo na masikini zaidi ya sisi inafanikiwa kwanini sisi tushindwe?.Angola wametangulia kufikiri kama hawajatuzidi kufikiri.Angola si nchi ya kwanza kufanikiwa,hapo awali nao walikua na akili zilizoganda kama zetu.Waliamua kufikiri tofauti na hatima yake wakafanikiwa mpaka kufuzu kombe la dunia mwaka 2006.Labda tff hawajasikia walichofanya angola pia hawajasoma wala kuona walichokifanya hawa jirani zetu.
                    Tff wamesahau kuwa hakuna jipya kwenye soka.Tff hawajui kuwa timu zote zilizofanikiwa nazo zilijifunza kwa waliowatangulia kufanikiwa.Tanzania tunao majirani waliofanikiwa lakini tunaogopa kuwaoigia chabo ili nasisi tufaulu.Hawakumbuki hata timu zilizofanikiwa nazo zilipiga chabo na zikafanikiwa.Hao Angola kwenye mafanikio yao walikopi kila kitu kutoka kwa wareno.Nchi kama senegal na mali zilikopi kila kitu kutoka kwa wafaransa,sijui  Tff yangu inasubiri nini? Dunia ya sasa hauhitaji kutumia akili nyingi ili kufanikiwa.Haswa huu ulimwengu wetu wa dijitali kila kitu kinajieleza chenyewe.Tumeshindwa kugundua, tutashindwaje hata kuhamisha majibu kwenye karatasi ya jirani ilihali macho tunayo.
                    Tff haina haja ya kwenda kujifunza Brazil au Ujerumani kabla ya kujifunza kwa majirani.Wanachohitaji watanzania kwa sasa ni kupiga hatua moja mbele kama walivyofanya majirani zetu mfano Angola, Ghana na Nigeria.Tff inabidi ikajifunze kutoka kwenye nchi hizo kwanza na kujua ni njia gani nchi hizo wametumia kufika hapa walipo.Ikiwezekana tff wakopi mfumo mzima wa uendeshaji soka wanaotumia nchi hizo na kuhamishia nchini.Hakika tutafanikiwa kwenye ubunifu huu wa kukopi.Nafikiri  hii ndio itakua njia rahisi kwetu kufikia mafanikio yetu.

                                                           

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MWANAFUNZI SHUJAA HAOGOPI KUPIGA CHABO Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top