728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, September 06, 2014

    SIMBA USIPIME YAIUA GOR MAHIA 3-0 TAIFA, KIONGERA NI SHEEEEDAH!!



    Habari na Paul Manjale

    Klabu ya Simaba imewapa zawadi ya wikendi mashabiki wake baada ya jioni ya leo kuibamiza klabu ya Gor Mahia ya Kenya kwa jumla ya magoli 3-0 katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki uliopigwa katika dimba la uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.

    Klabu ya Simba ambayo mwezi uliopita ilipokea kichapo cha mbwa mwizi toka kwa klabu ya Zesco ya Zambia iliuanza mchezo wa leo kwa umakini mkubwa lakini haikuweza kupata bao lolote katika kipindi cha kwanza kutokana na washambuliaji wake kushindwa kuzitumia nafasi walizozipata.
    Kiongera akishangilia goli dhidi ya Gor Mahia (Picha na bin zubery)


    Baada yakuanza kwa  kipindi cha pili klabu ya Simba ilionekana kuchangamka zaidi na kulisakama lango la Gor Mahia kama nyuki na kufanikiwa kupata magoli matatu huku mshambuliaji wake mpya toka Kenya Paul Kiongera akiifunga magoli mawili klabu yake hiyo ya zamani huku Ramadhan Singano maarufu kama Messi akifunga goli moja.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    1 comments:

    Item Reviewed: SIMBA USIPIME YAIUA GOR MAHIA 3-0 TAIFA, KIONGERA NI SHEEEEDAH!! Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top