728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, September 12, 2014

    PATO AILAUMU AC MILAN KWA KUHARIBU SOKA YAKE




    Mshambuliaji wa zamani wa klabu ya Ac Milan maarufu kama Rossoneri Mbrazil Alexander Pato ambaye kwa kwasasa anakipiga na klabu ya nyumbani kwao ya Sao Paulo ameilaumu klabu hiyo ya jiji la Milan kuwa ndiyo sababu ya kuharibu soka yake kutokana na majeruhi ya mara kwa mara aliyokuwa akiyapata.
    Pato akiwa na jezi ya Sao Paulo


    Pato ambaye allichezea Milan jumla ya michezo 117 na kufanikiwa kufunga jumla ya magoli 51 kati ya mwaka 2007 na 2012 akifanya mahojiano na kituo kimoja cha habari cha nchini Brazil amesema Ac Milan haikujali afya yake na badala yake ilimuwahisha kurudi uwanjani hata kabla hajapona vizuri.
    Pato akiwa na jezi ya Ac Milan


    Anasema “Nilipoanza kupata majeruhi nilisafiri karibu dunia nzima kwa ajili ya matibabu,lakini tatizo lilikuwa ni muda wa matibabu/kupona,niliwahishwa kurejeshwa kiwanjani.Klabu iliangalia maslahi yake tu huku ikiiacha afya yangu ikiteketea na hatimaye soka yangu kushuka.
    Pato akiwa na jezi ya Brazil


    “Hii imebainika baada ya vipimo nilivyofanyiwa hapa Brazil na kugundulika kuwa tatizo halikuwa langu.Huu ni msimu wangu wa pili hapa nikiwa na vilabu ya Corinthias na Sao Paulo sijapata majeruhi yoyote kwasababu afya yangu inaangaliwa.Alimaliza Pato
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: PATO AILAUMU AC MILAN KWA KUHARIBU SOKA YAKE Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top