728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, September 11, 2014

    NEWCASTLE YAWEKWA SOKONI,PARDEW APEWA MECHI MBILI KUOKOA KIBARUA CHAKE




    Mmiliki wa klabu ya Newcastle United inayoshiriki ligi kuu ya Epl Mike Ashley anafikiria kuipiga bei klabu hiyo inayotumia dimba la St.James Park kwa mechi zake za nyumbani ili aweze kuwa huru kuinunua klabu ya Rangers ya Scotland.
    Mike Ashley


    Ashley ambaye aliinunua Newcastle United mwaka 2007 kwa kitita cha paundi milioni 134 anapanga kuipiga bei klabu hiyo kwa paundi milioni 230 amekuwa katika mvutano wa mara kwa mara na mashabiki wa klabu hiyo hasa katika masuala mazima ya uendeshaji wa klabu na usajili wa wachezaji.

    Mmiliki huyo ambaye tayari ameshafanikiwa kujipenyeza na hatimaye kumiliki hisa kadhaa za umiliki wa uwanja wa Ibrox unaotumiwa na klabu ya Rangers kwa mechi zake za nyumbani anaona njia pekee ya kuachana na misuguano ya mara kwa mara na mashabiki wa Newcastle ni kuiuza klabu hiyo na kuinunua Rangers na hatimaye kuirejesha ligi ya mabingwa.
    Wachezaji wa Newcastle wakipambana na Gervinho


    Rangers ambayo kwa miaka mitatu mfululizo imekuwa ikikabiliwa na hali mbaya ya kiuchumi hata kufikia kushushwa daraja inaonekana kama ni jibu kwa Mike Ashley ambaye kiu na ndoto yake kubwa imekuwa ni kumiliki timu inayoshiriki ligi ya mabingwa.Kwakuwa shirikisho la vyama vya soka barani Ulaya Uefa haliruhusu mmiliki mmoja kuwa na timu mbili katika michuano iliyo chini yake Ashley hana budi zaidi ya kuachana na Newcastle United.

    Wakati huohuo Mike Ashley amempa mechi mbili tu kocha wa timu hiyo Alain Pardew ili kuokoa kibarua chache vinginevyo atamtimua mara moja.Pardew ambaye mwaka 2012 alipewa mkataba mrefu wa miaka minane kuendelea kukinoa kikosi hicho ameshindwa kushinda mchezo wowote kati ya mitatu ya ligi akiwa na klabu hiyo ya St.James Park msimu huu.
    Alan Pardew kocha wa Newcastle


    Kwa mujibu wa Ashley mechi zitakazomuokoa au kumuangamiza Pardew ni ile ya jumamosi dhidi ya Southampton na ile itakayofuata dhidi ya Hull City.Mapema wiki iliyopita Mike Ashley alianza kumshambulia kocha huyo kwa kumwambia kuwa hakustahiri kupanga wachezaji watano wa kikosi cha kwanza katika mchezo wa kombe la Capital One dhidi ya timu kibonde ya Gillingham.Pia mmiliki huyo ambaye ametumia paundi milioni 35 katika usajili wa nyota tisa klabuni hapo anaona kwamba Pardew hana kisingizio cha kuendelea kufanya vibaya na badala yake ahakikishe anashinda michezo hiyo miwili muhimu.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: NEWCASTLE YAWEKWA SOKONI,PARDEW APEWA MECHI MBILI KUOKOA KIBARUA CHAKE Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top