728x90 AdSpace

Saturday, September 06, 2014

NASRI:LIVERPOOL SIYO TISHIO TENA




Habari na Paul Manjale

Kiungo wa klabu ya Manchester City Mfaransa Samir Nasri amesema klabu ya Liverpool haitokuwa tena tishio msimu huu katika mbio za kuwania ubingwa wa Epl kama ilivyokuwa msimu uliopita ambapo ilimaliza ikiwa nafasi ya pili pointi mbili nyuma ya City waliotwaa ubingwa huo siku ya mwisho.
Nasri akiwa na taji la Epl


Badala yake Nasri amevipa nafasi vilabu vya Chelsea na Manchester United kutoa upinzani mkubwa kwa klabu yake msimu huu.Nasri anadhani kuwemo kwa Liverpool katika michuano ya ligi ya mabingwa na kuondoka kwa mshambuliaji wake mahiri Louis Suarez aliyetimkia klabu ya Barcelona kutaidhorotesha klabu hiyo kwa kiasi kikubwa.
Nasri akiwajibika uwanjani


Aliongeza “Chelsea walikuwa na kikosi kizuri msimu uliopita lakini tatizo lao lilikuwa n katika safu yake ya ushambuliaji ambayo kwa sasa imepata suluhisho baada ya kutua kwa mshambuliaji Diego Costa.Manchester United bado naipa nafasi ya kufanya vizuri licha ya kuanza vibaya michezo yake ya ligi.Kitakachoisaidia United ni  usajili mkubwa na mzuri ilioufanya pamoja  na kutokuwa na michuano mingi msimu huu.Arsenal bado siwapi nafasi kwani bado wana mapungufu makubwa katika kikosi chao. Alimaliza nyota huyo
Nasri akifanya mazoezi kabla ya mchezo wa ligi ya mabingwa

  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Post a Comment

Item Reviewed: NASRI:LIVERPOOL SIYO TISHIO TENA Rating: 5 Reviewed By: Unknown