728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, September 08, 2014

    FALCAO AISHUKURU MONACO KUKUBALI ATUE UNITED




    Habari na Paul Manjale

    Mshambuliaji mpya wa klabu ya Manchester United Mcolombia Radamel Falcao Garcia Zarate “El Tigre” ameishukuru klabu yake ya zamani ya Monaco kwa kukubali kumwachia atue katika klabu ya  Manchester United kwa uhamisho wa mkopo wa msimu mmoja wenye kipengele cha kuwa wa kudumu hapo baadae.


    Akiongea na mtandao wa Telefoot Falcao amesema “Nataka kuwashukuru watu wa Ufaransa kwa kuniunga mkono kwa kipindi chote nilichokuwa hapa”.

    “Binti yangu alizaliwa  hapa hivyo Monaco na  Ufaransa kwa pamoja zitabaki kuwa moyoni mwangu”

    “Nataka kuwashukuru watu wa Monaco kwa kunisaidia katika kipindi chote pamoja na kunipa nafasi ya kutua Manchester United”


    Wakati huohuo klabu ya Manchester United imetupilia mbali uvumi ulioenezwa juu ya umri halisi wa nyota wake huyo mpya raia wa Colombia na kusema  wanaamini kuwa mchezaji huyo ana umri wa miaka 28 na siyo 30 kama ilivyovumishwa na vyombo mbalimbali vya habari hapo nyuma.


    United kupitia msemaji wake mkuu imesema haishitushwi na uvumi huo badala yake inaamini kile kilichoandikwa katika hati ya kusafiria ya nyota huyo ambayo inaonyesha kuwa Falcao alizaliwa tarehe 10 february mwaka 1986 na siyo vinginevyo.

    Hivi karibuni kuliibuka uvumi kuwa Falcao alipunguza miaka miwili toka katika umri wake halisi ili apate nafasi ya kucheza katika fainali za kombe la dunia la vijana chini ya miaka 20 mwaka2005.Mwaka 2012 shule moja aliyosoma Falcao ilivujisha taarifa zikisema kuwa nyota huyo alizaliwa mwaka 1984 hatua iliyopelekea familia yake kuonyesha kwenye vyombo vya habari vyeti vya kuzaliwa vya nyota huyo mwenye jicho la goli.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: FALCAO AISHUKURU MONACO KUKUBALI ATUE UNITED Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top