728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, September 06, 2014

    ARSENAL YAMUWINDA YEPEZ AONGEZE NGUVU KIKOSINI



    Habari na Paul Manjale
    0717 70 55 48

    Ikiwa hata wiki moja haijaisha tangu dirisha la usajili lifungwe nchini England na sehemu nyingine duniani kocha wa klabu ya Arsenal Mfaransa Arsene Wenger ameendelea na harakati za kukiimarisha kikosi chake ili kiweze kufanya vizuri katika michuano yake mbalimbali ya ndani na nnje.


    Akiwa amegungua mapema kuwa kosa la kutosajili walinzi wa kutosha litamletea balaa mbele ya safari tayari kocha huyo ameanza kumfukuzia mlinzi mkongwe na nahodha wa timu ya taifa ya Colombia Mario Yepez mwenye umri wa miaka 38.


    Mario Yepez ambaye kwa sasa ni mchezaji huru baada ya kuachwa na klabu yake ya zamani ya Atalanta na Ac Milan vinayoshiriki ligi ya Seria A ya Italia aliiongoza timu yake ya taifa ya Colombia kufika robo fainali ya kombe la dunia nchini Brazil na kutolewa na wenyeji kwa magoli 2-1.



    Habari kutoka vyazo mbalimbali zinasema Arsene Wenger anataka kumpa nyota huyo mkongwe mkataba wa mwaka mmoja ili kuimarisha safu yake ya ulinzi wa kati iliyo chini ya Laurent Koscienly,Per Mertesacker na kinda Calum Chambers.


    Kuja kwa Yepez Arsenal kutamfanya nyota huyo kufikisha miaka 14 ya kucheza soka barani Ulaya huku 10 mingine akiitumia kucheza barani Amerika ya kusini Colombia na kwingineko


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: ARSENAL YAMUWINDA YEPEZ AONGEZE NGUVU KIKOSINI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top