728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, September 29, 2014

    RODGERS:BALOTELLI AMEANZA KUKUA



    Kocha mkuu wa klabu ya Liverpool Brendan Rodgers amemwagia sifa lukuki nyota wake Mario Balotelli kufuatia mwenendo mzuri anaoendelea kuuonyesha nje na ndani ya uwanja hasa katika mchezo wa jumamosi dhidi ya Everton.



    Rodgers amesifia mwenendo huo hasa baada ya nyota huyo kuonekana mtulivu licha ya kufanyiwa madhambi ya mara kwa mara na wachezaji wa Everton yaliyokuwa na lengo la kumkera ili achukie na kulipiza.Akifanya mahojiano
    baada ya mchezo huo Rodgers amesema


    “Anahitaji kuweka akili yake mchezoni kila mara na hilo nilimwambia mapema tu.Hii ni mechi ambayo joto lake huwa liko juu sana na huwa ngumu.Kiujumla alicheza vizuri mchezo huo ukianzia kujituma mpaka nidhamu yake vyote vilikuwa sawia,vilivutia na ilionekana kama angefunga goli.Nimehuzunika kwakuwa hakupata bahati ya kufunga lakini kama ataendelea hivi magoli hayako mbali atafunga tu.Tangu atue hapa amekuwa akiendelea vizuri,vizuri sana.Alimaliza kocha huyo kumwagia sifa nyota huyo ambaye bado hajafanikiwa kufunga bao lolote katika ligi ya Epl.
    Balotelli akikunjana na aliyekuwa kocha wake Roberto Manchini





    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: RODGERS:BALOTELLI AMEANZA KUKUA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top