728x90 AdSpace

Monday, September 08, 2014

SANOGO:MAGOLI YATAKUJA TU,WELBECK ASITEGEMEE MTEREMKO



Habari na Paul Manjale

Mshambuliaji wa klabu ya Arsenal anayepambana kuzigusa nyavu za adui japo kwa goli moja tu Mfaransa Yaya Sanogo ameibuka na kujitetea dhidi ya mashabiki na wadau mbalimbali wa mpira wanaodai kinda huyo si lilote si chochote klabuni hapo.
Sanogo akishangilia goli dhidi ya Benfica katika michuano ya Emirates


Sanogo  akiongea na jarida la L ‘Equipe la nchini Ufaransa amesema “Unapotoka moja kwa moja ligi daraja la pili Ufaransa (ligue 2)  na ukakutana na mtu kama vicent Kompany  kwa kweli inakuwa siyo kazi rahisi. Kwasasa najiona nimepiga hatua.Unajua unapofanya mazoezi na wachezaji mahiri uwezo wako unaongezeka na unapocheza mechi kubwa unapata uzoefu”
Vicent Kompany mmoja kati ya walinzi wanaomnyima usingizi Yaya Sanogo


Sanogo aliongeza “Upokuwa na miaka 21 siyo rahisi sana  kucheza nafasi ya ushambuliaji katika klabu kama Arsenal.Unahitaji kujituma sana ili uweze kuonyesha thamani yako.Mashabiki wanajua nimefunga magoli mengi sana nikiwa na vikosi vya vijana.
Enzi za Sanogo katika klabu ya Auxerre


Wanataka nianze kufunga lakini nawaahidi siku nikifunga goli langu la kwanza kutakuwa hakuna wa kunizuia tena itakuwa ni magoli na mimi,mimi na magoli”.

Pia Sanogo amemuonya nyota mpya wa klabu hiyo aliyesajiliwa hivi karibuni Danny Welbeck kuwa asitegemee kuanza moja kwa moja katika kikosi cha kwanza cha Arsenal na badala yake ategemee ushindani mkubwa toka kwake.
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Post a Comment

Item Reviewed: SANOGO:MAGOLI YATAKUJA TU,WELBECK ASITEGEMEE MTEREMKO Rating: 5 Reviewed By: Unknown