728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, September 05, 2014

    NAMBA ZA JEZI NA MAANA ZAKE



    Imeandaliwa na Paul Manjale
    0717 70 55 48
    paul.manjale@yahoo.com

    Huenda ukawa na maswali mengi sana juu ya baadhi ya namba zilizoko migongoni mwa baadhi ya wacheza soka duniani.Wapo wanaopenda kuvaa jezi zenye namba yoyote ile migongoni mwao lakini wapo ambao bila jezi namba fulani maisha huwa ni ya tabu na magumu sana kwao.

    Hivi umeshawahi kujiuliza kwanini mchezaji fulani anavaa jezi namba fulani ambayo wewe kwako inaweza kuonekana ni kituko?Ndiyo kwako ni kituko ila kwake habari ni tofauti kidogo,kuna kitu amekilenga hapo wala hafanyi hivyo kwa ajili ya kumkera yoyote bali ni kuifurahisha nafsi yake na maisha yaendelee.

    Leo nimeona siyo vibaya nikizungumzia baadhi ya namba na maana zake ili kujibu maswali lukuki yaliyoko mitaani kwetu kutokana na kila mtu kuwa na majibu yake ambayo kidogo ni tofauti na ukweli wenyewe.Wafuatao wanajibu maswali hayo!!

    1.       Mario Balotelli:Je,ni kwanini anapenda kuvaa jezi no 45 katika kila klabu anayokwenda?
    Wakati Mario anakuwa na kuanza kupenyeza katika kikosi cha vijana cha klabu ya Inter Milan ya Italia aliambiwa achague kuvaa jezi kati ya no 36-50 akachagua no 45.Hii ni kwasababu 4+5=9 ambayo ni nafasi anayoicheza uwanjani na kufanikiwa kufunga magoli katika mechi nne mfululizo akiwa na kikosi cha vijana cha Inter Milan.Hivyo akaamini kuwa hiyo ni jezi yenye bahati kwake na ndiyo maana kila klabu anayokwenda Balotelli huanza kuulizia jezi yake no 45 kama ipo.


    Ronaldinho (80),Andriy Shevchenko (76),Mathieu Flamini (84)
    Mwaka 2008-09 wakati klabu ya Ac Milan inawasajili nyota hawa watatu namba zao vipenzi zilikuwa tayari zimeshachukuliwa na wachezaji waliokuwepo klabuni hapo.Unajua nini kilifanyika?Hakuna mchezaji/wachezaji waliokubali kuwapa jezi zao nyota hao wapya hiyo hivyo iliwabidi nyota hao kuchagua jezi kulingana na umri wao wa kuzaliwa.


    Bixente Lizarazu (69)
    Mchezaji wa zamani wa timu ta taifa ya Ufaransa aliichezea klabu ya Bayern Munich akivalia jezi no 69 kwasababu alizaliwa mwaka 1969 na urefu wake ulikuwa ni 169.


    Clint Dempsey (2)
    Mchezaji na nahodha  wa timu ya taifa ya Marekani aliichezea klabu ya Fulham akivalia jezi no 23 lakini alipohamia klabu ya Tottenham Hotspurs alichagua jezi no 2 kama kielelezo kuwa mbali ya soka pia ana ajira nyingine ya pili ambayo ni kufanya muziki wa kufoka foka yaani rap na huko anafahamika kwa jina la Deuce

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: NAMBA ZA JEZI NA MAANA ZAKE Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top