728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, September 02, 2014

    MIKE PHELAN:KUUZWA KWA WELBECK NI TUSI KWA MANCHESTER UNITED




    Paul Manjale
    0717 705548

    Aliyekuwa kocha msaidizi wa klabu ya Manchester United Mike Phelan amesema kitendo cha klabu hiyo kumuuza mshambuliaji Danny Welbeck  kwenda klabu ya Arsenal ni kuua utambulisho wa klabu hiyo kongwe na maarufu zaidi.


    Phelan ambaye alikuwa msaidizi namba mbili wa kocha Alex Ferguson toka mwaka 2008-2013 ameiambia BBC “Welbeck amekuwa sehemu ya utambulisho wa Manchester United ambao umevunjwa.Nini kitatokea siku za usoni ,hakuna anayejua lakini tayari utambulisho huo umeshavunjwa.”

    Phelan aliongeza “Kila jambo huwa lina mwanzo wake labda huu ndiyo mwanzo mpya wa kufanya vitu klabuni na labda ndivyo mpira unakoelekea.Je,ni bora kutazama sasa kuliko mbeleni?alihoji kocha huyo. 

    Akikikumbuka kizazi cha akina David Beckham,Nick Butt,Paul Scholes,Garry na Phil Neville kilichobatizwa jina na kuitwa ‘Class of 92’ na kuja kutawala anga la soka ya England na dunia Phelan anaona ujio wa nyota kama Angel di Maria,Radamel Falcao,Marcos Rojo,Ander Herrera klabuni hapo ni kuua shule ya vipaji iliyoko klabuni hapo.

    Ni ngumu kwasababu vijana ndiyo huja na kuwa msaada mbeleni ,tunapaswa kuanzia sehemu fulani na kutumaini kuwa zao hilo la vijana litakuja kuwa ni msaada katika ligi kuu”.

    Pia Phelan amesema Welbeck atafanikiwa  Arsenal  “Yupo katika sehemu ambayo anaweza kucheza katika sehemu aitakayo na ninadhani hiyo ndiyo sababu iliyofanya achague kucheza hapo kwa sababu anaamini atacheza nafasi aipendayo,ambayo ni ushambuliaji.

    Klabu kama Arsenal ni klabu nzuri,ni klabu inayoendeshwa vizuri.Kama unataka kuchagua klabu ya mpira wa miguu basi Arsenal ndiyo jibu kwa mchezaji”.


    .
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MIKE PHELAN:KUUZWA KWA WELBECK NI TUSI KWA MANCHESTER UNITED Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top