728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, September 04, 2014

    JASON NONO MAYELE:MCONGO WA CHIEVO ALIYEKUFA AKILIWAHI BASI LA KLABU




    KUMBUKUMBU MICHEZONI
    Imeandaliwa na Paul Manjale
                         0717 70 55 48

    Jason Mayele huenda siyo jina maarufu sana masikioni na machoni mwa wapenzi wa soka Tanzania kama ilivyo kwa majina mengine ya wachezaji toka Congo DRC kama Lomana LuaLua,Tresor Mputu na wengineo wengi.
    Mayele akifanya vitu vyake dimbabi dhidi ya Juventus


    Mwili wa Mayele baada ya ajali
    Lakini katika jiji la Chievo nchini Italia na Congo kwenyewe Jason Nono Mayele ni mmoja katika ya nyota maarufu na wanaoheshimika zaidi kila inapoitwa leo,siyo tu kwasababu ya kifo chake bali pia kwa mchango wake kwa klabu yake ya Chievo na timu yake ya taifa ya Congo.




    Je,Jason Mayele ni nani?

    Jason Nono Mayele kama anavyofahamika zaidi katika mitaa mingi ya Bussolengo,Italia na Congo alizaliwa tarehe 4 januari 1976 huko Kinshasa na kufariki tarehe 2 machi 2002 huko Bussolengo Italia.

    Kabla ya kifo chake Mayele aliyemudu kucheza vyema nafasi za ushambuliaji na winga alifanikiwa kuchezea kwa mafanikio  vilabu vya Brunoy (1991-1993),LB Chateauroux  ya Ufaransa (1993-1999),Cagliari (1999-2001) na mwisho Chievo (2001-2002).

    Kifo chake

    Mayele aliyekuwa mmoja kati ya nyota wa Chievo walioweka rekodi ya kuipeleka klabu hiyo katika michuano ya Ulaya katika msimu wake wa kwanza tu katika ligi ya Seria A alifariki akiwa na miaka 26 katika ajari mbaya ya gari.
    Gari alilokuwemo Jason Mayele likiwa limeharibika vibaya


     Mayele aliyekuwa akiliwahi basi la klabu yake la Chievo kwa ajili ya kwenda kwenye mchezo wa ugenini  wa ligi ya Seria A dhidi ya klabu ya Parma, gari dogo alilokuwa akilitumia liligongana uso kwa uso na gari jingine na kukatisha uhai wa nyota huyo kutokana na majeraha makubwa aliyoyapata katika sehemu mbalimbali za mwili wake wakati akiwahishwa hospitali ya karibu katika mji wa Verona.
     


    Jezi yake yastaafishwa

    Uongozi wa klabu ya Chievo uliamua kuistaafisha jezi no 30 iliyokuwa ikivaliwa na Jason Mayele ili kutoa heshima kwa nyota huyo aliyekufa katika mapambano ya kuitetea klabu hiyo.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    1 comments:

    Item Reviewed: JASON NONO MAYELE:MCONGO WA CHIEVO ALIYEKUFA AKILIWAHI BASI LA KLABU Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top