728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, September 26, 2014

    LIVERPOOL MSINIPOTEZEE MWANANGU

                                                               MAKALA YA LEO
    Na Mkubwa Kambi
    Liverpool msinipotezee mwanangu!! Ninaipenda kweli Liverpool lakini mwanangu nampenda zaidi, hii ni kinyume na mwanangu mwenyewe, yeye anaonekana kuipenda zaidi Liverpool kuliko anavyonipenda mimi (ni utoto tu akikua ataacha), ukiona siku amenibeep basi anaomba kibali akaitazame Liverpool kwenye Luninga.

     Liverpool bado haijakaa vyema, na hakuna mpaka sasa anayejua tatizo la Liverpool liko wapi? mbaya zaidi hata Brendan Rodgers pia hajui tatizo la timu yake!!, bench la ufundi la Liverpool hawajui tatizo la timu yao!!, mashabiki damu wa Liverpool hawajui tatizo la timu yao!! Ingia kwenye mitandao yoote ya Liverpool hivi sasa wanagombana tu wenyewe kwa wenyewe, wale wenye mioyo ya chura (mioyo isiyo na uvumilivu) ndio kabisa kila kukicha ni kulaumu. 

    Bahati mbaya zaidi Liverpool hata hapa Tanzania ina washabiki wenye kuheshimika sana (amini maneno yangu) washabiki ambao hawana kelele, mashabiki ambao ni Die Hard,Hata Mr. Liverpool Ezekiel Kamwaga naye simuoni tena akiandika kwa mbwembwe kuhusu Liver yeke!! hata wachambuzi wetu wa magazeti kwa kuwa nao ni wanajamii wanaogopa kuandika ukweli kuhusu Liverpool nadhani wanatuonea haya! Si marafiki zatu na wanatuheshimu, lakini lingine wanajua kuwa Liverpool haitabiriki inaweza kuamka wakati wowote! Unabisha? kwani ulijua kama mwaka jana wangeweza kuwa juu ya timu yako iliyosheheni wachezaji World Class, timu yako yenye mashabiki wenye kelele kila kona?!!

     Baada ya kuitazama Liverpool kwa jicho huru, baada ya kuamua kuweka pembeni mahaba niue nimepata mwanga kidogo wa kugundua matatizo ya Liverpool. 

    1. Nafasi waliyoishika msimu uliopita;- Kama nilivyotangulia kusema awali nafasi waliyoikamata Liverpool mwaka jana ilikuja kama surprise japo ilisababishwa na jitihada za pamoja kama timu kuanzia wachezaji, benchi la ufundi na support ya Empire Of The Kop L.F.C ambayo huwa haipotei, kwa kushika nafasi ya pili kwenye ligi na kuwa mpigania ubingwa hadi mechi ya mwisho kila mmoja ndani ya Liverpool nafasi pekee iliyopo kwenye fikra zao ni ubingwa ikishindikana kubaki Top 4 na ili jambo hilo liwezekane hii timu ilihitajika ianze ligi ikiwa ile ile iliyomaliza ligi bila kumpoteza mchezaji hata mmoja, kama ni wachezaji wapya walipaswa kuingia pole pole kwa kumbadilisha mchezaji mmoja mmoja kwa awamu.


     2. Kutokuwa na First Eleven:- Liverpool hadi sasa baada ya kucheza mechi nne za EPl na moja ya ligi ya mabingwa bado haina First Eleven, wachezaji wenye uhakika wa namba ni watano tu pamoja na Nahodha aliyechoka, (Simon Mignolet, Martin Skirtel, Alberto Moreno, Steering, na Daniel Sturridge) wengine wote hujui nani ataanza leo nani ataingia sub hili ni tatizo kubwa pia kwani inaonekana limewaingia hata wachezaji wenyewe hivyo kukosa maandalizi ya kiakili ya mchezo unaofuata, mchezaji anapojua atakuwemo kwenye kikosi cha juma lijalo humfanya aisumbue akili yake kuwa kitu gani bora atakifanya kwa faida yake na faida ya timu kiujumla.

     3) Kikosi kujaa wachezaji Standard:- Liverpool ilimaliza msimu uliopita ikiwa na wachezaji World Class wawili tu, Steven George Gerrard na Luis Suarez ambacho ilipaswa kupigania ni kuongeza watu wa kaliba hiyo japo wawili bahati mbaya kwao ikawalazimu kumuuza LUIS SUAREZ ambaye ndiye alikuwa roho ya timu na wakaingiza wachezaji karibu wanane ambao ni wachezaji wa kawaida (Ukiondoa Balloteli pekee), hii imeigharimu sana timu, unapokuwa na wachezaji wa aina hii inakuwa ni ngumu kupata matokeo kwenye mchezo ambao timu pinzani imewazidi mbinu za kimchezo, faida ya kuwa na wachezaji ambao ni World Class ni pale timu inapozidiwa mbinu za kimchezo ndipo vipaji binafsi pamoja na uzoefu vinapofanya kazi ya kuamua matokeo Liverpool ya sasa inamtegemea Steering pekee ndio afanye kazi hii pia faida nyingine wachezaji hawa huingia moja kwa moja katika kikosi cha kwanza unless otherwise wakute wachezaji wa kaliba yao kikosini, .

     4) Kukosekana mhimili wa timu (beki):- Nyumba imara zote duniani huanza kujengwa msingi ulio imara na kwenye timu za soka timu ii iwe imara huitaji kuwa na beki imara, msimu uliopita Liverpool haikuwa na beki imara! ilipata bahati ya kuwa na kiongozi imara kwenye safu ya ulinzi Martin Skirtel aliyekuwa na wasaidizi wawili pembeni yake Agger na Mamadou Sakho ambao walijenga safu nzuri sana pongezi kwake kijana Flanagan ambaye alikuja kuisakafia vyema hii ngome, msimu huu kuna maingizo matatu mapya kule nyuma, Manquillo, Moreno na Lovren katika hali ya kawaida wanahitaji kupewa muda ili wajenge ukuta ulioimara, je ligi inawasubiri wao? jibu unalo wewe shabiki wa Liverpool, Bahati mbaya zaidi timu imekosa kiungo mkabaji, kiungo mkabaji pekee aliyepo pale Liverpool ni Lucas Leiva bahati mbaya BR amepoteza uaminifu kwake.

     5) Majeruhi:- Hii nayo wakati mwingine ni mipango ya Mungu yeye anapanga sisi tunapangua, Flanagan, Sturridge, Coutinho, hata Skirtel wameingia kwenye group la wagonjwa, wachezaji hawa walimaliza ligi ya msimu uliopita wakiwa kwenye kikosi cha kwanza, timu inapokosa wachezaji wanne waliomaliza vyema msimu uliopita huku ikiwa na maingizo mapya karibu sita ni pigo kubwa, kwenye hili tuzidi kumba Mungu wachezaji wote wawe fit ili kumpa mwalimu chaguo sahihi. 

     Nini kifanyike?

     1) Katika sheria za soka wachezaji wa ndani wakifika saba timu inaruhusiwa kucheza mechi na hawa ndio wachezaji pekee wa Liverpool ambao Brendan Rodgers hapaswi kuwaweka bench kuwaweka bench labda wawe majeruhi (Moreno, Skirtel, Jordan Henderson, Steering, Coutinho, Sturridge na Balotelli) hapa ndipo msingi wa kujenga First eleven uanzie.

     2) Hili washabiki wengi wa Liverpool hawataki kulisikia, ndugu zangu, nguvu kitu cha kwisha, tulikuwa na kina Mohammed Ally,Mike Tyson, n.k leo hii wako wapi kama ingekuwa ni draft ama bao hadi hii leo tungeendelea kuwa nao. Steven Gerrald anapaswa kuchaguliwa baadhi ya mechi, hasa kwa ile position anayoitumikia sasa hivi ni kumtafutia malipo ya uzeeni yasiyostahili, Brendan Rodgers weka Lucas pale, bahati mbaya msimu uliopita alikabiliwa na majeruhi mkabidgi majukumu pale ama la train Jordan Henderson aanze kuitumikia nafasi ile kwa style yake ya uchezaji ndani ya mechi nne tu atakuwa ameshayajua majukumu yake.

     3) Liverpool itengeneze mfumo wa kushambulia kupitia kwa Mario Balotelli, wachezaji wote wacheze kumzunguka yeye ni mtu mwenye miguu yenye macho, misuli yenye nguvu, mwepesi kupinduka anapoliona goli mwisho ni mshindani halisi, bahati mbaya sana hadi sasa mashuti karibu yote aliyopiga Balotelli kuelekea golini pamoja na magoli aliyofunga ni juhudi zake binafsi. Timu yoyote duniani ingemhitaji Balotelli ukiondoa kasoro zake ambazo ni Mungu pekee anayeweza kumuepusha nazo. Mwisho kabisa ule mpango wa kumnyakua Víctor Valdés ufanywe haraka ili Mignolet apate mshindani halisi, apate changamoto ya kutosha. Zaidi ya yote You will never walk alone.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: LIVERPOOL MSINIPOTEZEE MWANANGU Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top