728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, September 27, 2014

    LUKAKU:LIVERPOOL WANAFUNGIKA

    Mshambuliaji hatari wa klabu ya Everton Romelu Lukaku amesema klabu ya Liverpool ni kama vilabu vingine tu hivyo kufungika inawezekana.Lukaku ameyasema hayo kabla ya kuikabiri klabu hiyo katika mchezo wa watani wa jadi utakaopigwa katika dimba la Anfield leo jumamosi.


    Liverpool inaingia katika mchezo huo ikiwa imecheza jumla ya michezo mitano na kufungwa mitatu huku ikiwa imefanikiwa kushinda miwili pekee haionyeshi kumtia hofu yoyote Lukakau.

    Amesema “Kila mtu anaongea kuhusu Everton hakuna anayeongea kuhusu Liverpool.Wanafungika,siko hapa kukosoa.

    “Nawaheshimu Liverpool kama wao wanavyopaswa kutuheshimu sisi.Tuna kikosi kizuri ambacho naamini tukianza kushinda itakuwa vigumu kutuzuia.Mchezo huu ni muhimu kwetu kwani tunaweza kuanzia hapa kuandika historia mpya.Tumekuja Anfield mara sita,tumepoteza mara nne na kupata sare mara mbili nadhani huu ni wakati wetu kushinda”
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: LUKAKU:LIVERPOOL WANAFUNGIKA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top