728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, September 09, 2014

    BENATIA:SOKA IMENIOKOA NA MENGI




    Mlinzi mpya wa klabu ya Bayern Munich Mmorocco Mehdi Benatia (27) ambaye hivi karibuni ametua klabuni hapo kwa kitita cha euro 27 akitokea klabu ya As Roma ya Italia amesema bila ya mchezo wa soka hajui leo hii angekuwa wapi.


    Benatia ambaye ni zao la baba Mmorocco na mama Mualgeria alikulia pembezoni mwa jiji la Paris (Ufaransa) ambako takwimu za uharifu kwa mujibu wake  ziko juu mno,anasema soka  ndiyo ilikuwa njia pekee ya kumuweka mbali na matatizo hayo.


    Akifanya mahojiano na jarida la Kicker la nchini Ujerumani Benatia amesema 

    “Nisingeweza kuwa daktari au injiania,wazazi wangu hawakuwa na fedha za kutosha hivyo hakukuwa na jinsi ilibidi nitafute njia.Soka imeniokoa,sijui hali ingekuwaje nisingekuwa katika upande huu wa maisha”.


    Benatia aliibuliwa na wasaka vipaji vya soka maarufu kama scouts  akiwa na umri wa miaka 13 na kupelekwa katika shule zilizoko jijini humo ili kuendeleza kipaji chake .Akikumbuka tukio hilo Benatia anasema 

    “Niliondoka eneo lile na hilo lilikuwa ni jambo zuri kwangu.Soka ilikuwa ni muhimu mno.Kwa watoto wote pale soka ilikuwa ni njia ya kuachana na kila kilichoendelea pale.Sikufanya vizuri darasani,sikuwa msikivu ilikuwa ni eneo gumu sana kuishi nashukuru soka imeniokoa.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: BENATIA:SOKA IMENIOKOA NA MENGI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top