728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, September 09, 2014

    WILSHERE AWAOTA PIRLO NA MASCHERANO




    Kiungo wa kimataifa wa England Jack Wilshere amefurahishwa na kiwango alichokionyesha usiku wa jana katika mchezo wa kusaka tiketi ya kufuzu michuano ijayo ya Ulaya dhidi ya timu ya taifa ya Uswisi uliopigwa katika dimba la Jacob Park mjini Basel.


    Wilshere ambaye alicheza nafasi ya kiungo wa ulinzi ameelezea furaha yake kwa kusema 

    “ Nawapongeza wachezaji wenzangu kwa ushindi mkubwa wa bao 2-0 tulioupata dhidi ya wenyeji Uswisi kwakweli ulikuwa ni mchezo mgumu mno, wapinzani wetu walicheza kwa nguvu na maarifa makubwa sana”.


    Pia nina furaha kwa kucheza vizuri katika nafasi mpya niliyoagizwa kucheza na kocha Roy Hodgson kama kiungo wa ulinzi.Sikuwahi kuicheza nafasi hii kabla.Niliongea na kocha pamoja na Garry Neville kabla ya mchezo wakaniambia wanataka nicheze nafasi hiyo na nimeifurahia kwakweli”.

    “Ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kucheza nafasi hiyo nadhani baada ya mazoezi makali na kutazama video ya mchezo huo pamoja na za viungo mahiri kama Pirlo na Mascherano nitaimarika sana”


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: WILSHERE AWAOTA PIRLO NA MASCHERANO Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top