728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, September 15, 2014

    ARSENAL HOFU TUPU,DEBUCHY AHOFIWA KUWA NJE MIEZI MIWILI



    Klabu ya Arsenal huenda ikazikosa huduma za mlinzi wake wa kulia Mfaransa Mathieu Debuchy kwa muda wa miezi miwili au zaidi kufuatia maumivu ya kifundo cha mguu aliyoyapata katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Manchester City uliopigwa katika dimba la Emirates.


    Debuchy alitolewa nje kwa machela dakika ya 81 ya mchezo kufuatia kujikwaa na kuangua wakati akijaribu kumiliki mpira kulikopelekea kuumia kwa kifundo cha mguu wake wa kushoto.Vipimo vya awali vimeonyesha kuwa mlinzi huyo hajavunjika kama ilivyodhaniwa na badala yake vinasubiriwa vipimo vingine (scanning) ili kubaini ukubwa wa jeraha na muda wa matibabu ambao unahisiwa utakuwa kati ya miezi miwili mpaka mitatu.

    Kufuatia kuumia kwa Debuchy,Arsenal inabaki na walinzi watano wanaopaswa kuziba nafasi tano zilizoko katika idara hiyo huku kinda Calum Chambers akichukua jukumu la kucheza nafai ya ulinzi wa kulia katika mchezo wa jumanne wa ligi ya mabingwa dhidi ya Borussia Dortmund.


    Debuchy mbali ya kuukosa mchezo dhidi ya Dortmund pia atakozikosa mechi kadhaa za ligi zikiwemo dhidi ya Spurs na Chelsea pamoja na Galatasaray na Anderletch kwenye ligi ya mabingwa.

    Akizungumzia hilo kocha Wenger alisema “Hakuna mvunjiko wowote alioupata lakini ni jeraha kubwa.Ni baya na siyo zuri hata kidogo
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: ARSENAL HOFU TUPU,DEBUCHY AHOFIWA KUWA NJE MIEZI MIWILI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top