728x90 AdSpace

Monday, September 15, 2014

CASILLAS AKUBALI LAWAMA MADRID



Mlinda mlango wa klabu ya Real Madrid Iker Casillas amekubali  baadhi ya lawana zinazoelekezwa kwake toka kwa mashabiki wa klabu hiyo baada ya kipigo cha goli 2-1 toka kwa wapinzani wao wa mji mmoja Atletico Madrid katika mchezo wa La Liga uliopigwa juzi jumamosi katika dimba la Santiago Bernabeau.


Casillas,33,ambaye siku hiyo alikuwa akicherekea kufikisha miaka 15 tangu aanze kuidakia timu hiyo alijikuta akianza kuyapata machungu ya mashabiki wa klabu hiyo baada ya wageni Atletico Madrid kutangulia kupata bao dakika ya 10 ya mchezo kwa kichwa cha karibu cha kiungo Tiago Mendez.Baada ya bao hilo mashabiki hao walianza kumzomea mlinda mlango huyo wakidai alipaswa kufanya kitu cha ziada badala ya kuruhusu bao ambalo wao wanaliona ni la kizembe.


Casillas ambaye ameichezea klabu hiyo michezo 684 akifanya mahojiano  na Canal Plus Tv alisema  

“Mashabiki ndiyo wenye kauli ya mwisho na wakifikiri wanapaswa  wakuzomee huna budi kukubali na kuheshimu mawazo yao.Ni haki yao na ninachopaswa kufanya ni kuwajibu kwa njia/namna niijuayo,kwa kucheza mpira”.

Akihojiwa kuhusu kuendelea kufungwa mipira ya kutenga (set pieces) Casillas alisema “Nalijua tatizo hilo ambalo kwa kiasi kikubwa linatokana na kupoteza kujiamini  kunakopolekea tuendelee kuruhusu magoli mengi ya set pieces,mimi kama mlinda mlango nawajibika kwa hilo.


“Nawajibika kwa hilo na ninapaswa kukubali baadhi ya lawama hizo.Kati yetu tunapaswa kulitatua tatizo hilo ambalo linakuwa siku hadi siku”.Alimaliza Casillas ambaye ameshaisaidia klabu hiyo kushinda mataji matatu ya ligi ya mabingwa,mataji mawili ya Copa del Rey na matano ya La Liga.
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Post a Comment

Item Reviewed: CASILLAS AKUBALI LAWAMA MADRID Rating: 5 Reviewed By: Unknown