728x90 AdSpace

  • Latest News

    Sunday, September 14, 2014

    VAN GAAL:VALENCIA JIFUNZE KIINGEREZA



    Kama unadhani ujio wa kocha Mdachi Lous Van Gaal katika klabu ya Manchester United ni wa mchezo mchezo tu basi sikia hii.

    Kocha huyo ambaye kiuhalisia ni mkali na asiyependa masihara hata kidogo amuibuka na mpya mapema wiki hii baada ya kuwanyoonyesha kidole cha shahada nyota wake wanaoongea Kihispania wakiongozwa na winga Antonio Valencia na kuwataka wajifunze lugha ya kiingereza haraka vinginevyo hali itakuwa mbaya kwao.



    Van gaal amefikia hatua hiyo ili kurahisisha mawasiliano kati yake na wachezaji wake ama wachezaji kwa wachezaji wakati wote wa mazoezi na mechi.Tayari kocha huyo ameshawaanzishia darasa maalumu nyota wake wageni ili kuhakikisha wanaimudu lugha hiyo adimu.Nyota ambao tayari wameshaanza makamuzi (kujifunza) ni Marcos Rojo na Angel di Maria ambao wameanza hatua ya awali kabisa yaani “beginners “hawa wanapata tuisheni mara mbili kwa wiki.Falcao,Herrera na David de Gea hawa kidogo wanajitahidi wameweka katua ya kati yaani “Intermediate”.  


    Inasemekana Antonio Valencia ambaye mpaka sasa ameshaishi England kwa miaka minane tangu atue nchini humo mwaka 2006 akiwa na miaka 20 tu hajawahi kufanya mahojiano (interview) kwa lugha ya kiingereza.Hii inatokana na tabia ya aibu aliyonayo nyota huyo mzaliwa wa Ecuador hata kufikia kumuomba Van gaal ampatie darasa la peke yake bila kuchanganyika na wenzake.




    Hatua hii ya Van gaal imepokelewa kwa mikono miwili na mashabiki wa klabu hiyo ambapo hapo awali walianza kuwa na mashaka na kule United ilikokuwa ikielekea na kuhisi kupotea kwa utambulisho wa klabu hiyo hasa baada ya kuleta nyota wengi wakubwa huku wazawa kama Danny Welbeck na Tom Cleverly wakionyeshwa mlango wa kutokea.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: VAN GAAL:VALENCIA JIFUNZE KIINGEREZA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top