728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, September 01, 2014

    TETESI ZA USAJILI JUMATATU YA LEO…..LOLOTE LINAWEZA KUTOKEA



    Paul Manjale
    0717705548

    Ikiwa leo ndiyo mwisho wa usajili barani ulaya pata kujua machache yatakayojili ndani ya saa kadhaa zijazo….

    STAMFORD BLIDGE: Klabu ya Chelsea imemtoa kwa mkopo kiungo wakeMdachi  Marco Van Ginkel  (21) kwenda klabu ya Ac Milan ya Italia wakati huo huo kiungo mwingine wa klabu hiyo Mscottland Islam Ferouz amerejea klabuni hapo  zikiwa ni saa 48 tu tangu atue kwa mkopo katika klabu ya Kylia Soveton Samara inayoshiriki ligi daraja la pili nchini Urusi kwa madai kuwa bado hakuwa tayari kuanza maisha mapya hapo baada ya awali  kupata tabu kuzoea England.


    EMIRATES:Kutoka gazeti kubwa na maarufu la michezo nchini Ureno O jogo habari zinasema kinda wa klabu ya Arsenal Joel Campbell ameomba kutimka klabuni hapo na kujiunga na klabu ya Benfica.O jogo linasema Campbell ameomba kuondoka baada ya kuhisi huenda kocha Arsene Wenger bado hayuko tayari kumtumia katika kipindi hiki.Hivi karibuni klabu ya Benfica ilifanya mawasiliano na klabu ya Arsenal kutaka kumsajili nyota huyo kwa uhamisho wa mkopo ama wa kudumu na kuwa tayari kulipa kitita cha Euro milioni 10. 

    ETIHAD:Mshambuliaji Alvaro Negredo amekubali kutua Valencia kwa mkataba wa mkopo wa msimu mmoja wenye kipengere cha uhamisho wa kudumu ili kumpisha mshambuliaji Radamel Falcao anayewaniwa kwa udi na uvumba na klabu ya Manchester City 

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: TETESI ZA USAJILI JUMATATU YA LEO…..LOLOTE LINAWEZA KUTOKEA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top