728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, September 02, 2014

    JE,UNAJUA JINA FALCAO LILIKOTOKA?SOMA HII



    Imetayarishwa na Paul Manjale
    0717 705548
     
    RADAMEL FALCAO GARCIA ZARATE

    Wakati dirisha la usajili likifungwa usiku wa septemba mosi gumzo kubwa England na duniani kote lilikuwa ni usajili wa mshambuliaji hatari raia wa Colombia Radamel Falcao Garcia Zarate  (El Tigre/mfalme wa ligi ndogo ya Ulaya maarufu kama Europa League) kutua klabu ya Manchester United kwa uhamisho wa mkopo wa msimu mmoja.


    Falcao ambaye alizaliwa tarehe 10 Februari 1986 huko Santa Marta,Colombia ni mtoto wa mchezaji wa  wa zamani wa nafasi ya ulinzi  wa timu ya taifa ya nchi hiyo Radamel Garcia.Falcao ametua Manchester United kwa ada  ya mkopo ya paundi milioni 6 huku kukiwa na kipengere cha kumsajili moja kwa moja mwishoni mwa msimu kwa kitita cha paundi milioni 43.5.


    Je,jina Falcao lilitoka wapi?
     Radamel alipewa jina Falcao na baba yake mzazi kutokana na mzazi huyo kuwa na mapenzi makubwa na nyota wa zamani wa nafasi ya kiungo wa timu ya taifa ya Brazil na klabu ya As Roma Paulo Roberto Falcao.Paul Roberto Falcao aliyetamba sana miaka ya 80s na kuwa mchezaji ghali zaidi kipindi Fulani inasadikika kuwa ni mmoja kati ya viungo bora zaidi timu ya taifa ya Brazil kuwahi kuwa nao.


    Je,baadhi ya makocha wanamzungumziaje?

    Fabio Capello “Radamel Falcao yuko daraja moja na nyota kama Lionel Messi na Christiano Ronaldo”……….
    Pep Guadiola “Falcao ni mchezaji wa ajabu,na ni mmoja kati ya wachezaji wenye vipaji vikubwa sana vya soka duniani”


    Afunga goli 5 peke yake katika mchezo mmoja wa La Liga.Ilikuwa ni desemba 9,2012 katika mchezo wa ligi uliopigwa katika dimba la Vicente Cardeloni ambapo Atletico Madrid walishinda jumla ya bao 6-0 huku Falcao akiweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza kufunga goli 5 ndani ya muongo mmoja katika mchezo mmoja wa ligi ya La Liga.

    Je,kipi kingine kilimvutia baada ya Monaco kumtaka?

    Mbali ya mshahara mzuri na mambo mengine  binafsi Falcao alisema “Nimetua Monaco kufuata nyayo za Thierry Henry ambaye alipita hapa na kuwa nyota mkubwa duniani.Nampenda sana Henry nimekuwa shabiki wake mkubwa hivyo uwepo wangu hapa ni kuenzi japo kidogo kile alichofanya na alikopitia”

    Je,goli lake la kwanza akiwa na timu ya taifa alilifunga akiwa na umri gani?

    Ilikuwa ni katika mchezo wa kombe la Kirin Cup uliopigwa huko Japan.Falcao alifunga goli pekee na la ushindi katika mchezo huo dhidi ya Montenegro.

    Je,alianza soka la ushindani akiwa na miaka mingapi?
      
    Falcao alinza kucheza soka katika timu ya daraja la pili nchini Colombia maarufu kama Categoria Primera B tarehe 28 Agasti 1999 akiwa na umri wa miaka 13 na siku 199 na kuweka rekodi ya kuwa mchezaji mdogo zaidi kuwa kucheza ligi ya kulipwa ya nchi hiyo.

    Februari 2001 Falcao alitua Argentina kuichezea klabu ya River Plate kwa dau la dola 500,000 na kuanza kukichezea kikosi cha vijana cha klabu hiyo kilichokuwa ligi daraja la nane kabla ya kupandishwa kikosi cha kwanza mwaka 2005 na kocha Leonardo Estrada.




    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: JE,UNAJUA JINA FALCAO LILIKOTOKA?SOMA HII Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top