728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, September 13, 2014

    PELE:PAMBANENI NA UBAGUZI KWA KUMUIGA DANI ALVES



    Habari na Paul Manjale
     
    Nyota wa zamani wa Brazil Pele amewataka wachezaji  wanaocheza ligi ya nchi hiyo kufuata mfano wa mlinzi wa kulia wa Barcelona Dani Alves katika mapambano yao dhidi ya ubaguzi wa rangi michezoni na kuacha kulikuza tatizo hilo kwenye vyombo vya habari .Hii imekuja kufuatia kufungiwa kwa klabu ya Gremio kutokana na vitendo  vichafu vya ubaguzi toka kwa mashabiki wake dhidi ya mlinda mlango mweusi wa Santos.


    Pele ameyazungumza hayo hivi karibuni kufuatia  kikundi cha mashabiki wa klabu ya Gremio ambao ni mabingwa mara nne wa taji la ligi maarufu kama Brazilian Cup (Copa Dos Brasil) ambalo ni taji la pili kwa ukubwa nchini  kumfanyia vitendo vya kibaguzi pamoja na kumuita nyani mlinda mlango wa klabu ya Santos,Mário Lúcio Costa Duarte,Aranha katika mchezo uliopigwa katika dimba la Arena Gremio  huko Porto Alegre na Santos kuibuka na ushindi wa goli 2-0.
    Aranha akilalamika kwa mwamuzi baada ya kubaguliwa na mashabiki wa Gremio


    Kufuatia kosa hilo mahakama ya michezo imeamua kuitoa mashindanoni klabu hiyo inayofundishwa na kocha Felipe Scolari pamoja na kuipiga faini ya dola 20,000 huku mwanamke  wenye umri wa miaka 23 aliyetambuliwa kuwa ndiye chanzo cha kadhia hiyo akifungiwa kujihusisha na masuala yote ya soka kwa miaka miwili.
    Aranha akiwa mazoezini


    Pele amesema “Mwaka jana,wakati Alves anaenda kupiga kona,kuna mtu alimtupia ndizi uwanjani.Aliimenya ndizi ile,kuila na akapiga kona ile.Hakuna aliyeongelea tena swala lile.Kilikuwa na kitendo cha ubaguzi.Nadhani kama Dani angeichukua ile ndizi na kuitupa,tungekuwa tunaliongelea tukio hilo mpaka leo.
    Mashabiki wa Gremio


    “Nafikiri Aranha alijivuruga kidogo baada ya kutaka kugombana na mashabiki wa Gremio.Kama ingekuwa ni kususa ama kulalamika kwa mwamuzi kila mara tangu nilipoanza kucheza soka hapa Brazil,Latin America na kwingineko,kila nilipokuwa nikifanyiwa vitendo vya kibaguzi basi kila mchezo ungekuwa unasimamishwa”.

    “Kuna wakati Santos ilikuwa na Dorval, ambaye alikuwa ni mweusi  akicheza winga,Pele alikuwa mweusi.Mengalivio  alikuwa mweusi  pamoja na Coutinho.Santos tulikuwa mabingwa wa dunia huku Pepe akiwa mzungu pekee katika kikosi kizima.Tulipokuwa tukicheza katika maeneo ya ndani ndani ya Brazil (vijijini) tulikuwa tukiitwa majina ya ajabu ajabu.Je,mliwahi kusikia habari zozote za ubaguzi wakati huo?Ni kwa sababu tulikuwa hatulitilii mkazo suala hilo.Unapoliongea sana jambo ndivyo unavyozidi kulikaribisha”.Alimaliza Pele
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: PELE:PAMBANENI NA UBAGUZI KWA KUMUIGA DANI ALVES Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top