728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, September 16, 2014

    FERDINAND:CHIPS ZILIMUONDOA MOYES UNITED



    Ama kweli dunia ina mambo!!kama huamini sikia hii.Mlinzi wa zamani wa klabu ya Manchester United Rio Ferdinand amesema moja kati ya sababu kubwa za kikosi cha United kuvurunda msimu uliopita ni kutokana na aliyekuwa kocha wao wakati ule David Moyes kuwapiga marufuku kula chips jioni kabla ya mechi.Upo?

    Hii ni moja katika ya tuhuma kibao dhidi ya David Moyes zilizoko katika kitabu cha Ferdinand kiitwacho 2sides ambacho kimeanzwa kuchapishwa kwenye gazeti la The Sun la Uingereza.
    Rio amesema “Ilikuwa ni desturi yetu kula Chips jioni kabla ya mechi lakini Moyes alipoingia aliuvunja utaratibu huo na hapo ndipo balaa lilipoanza.Jiulize nini kilitokea muda mfupi baada ya Moyes kutimuliwa na Ryan Giggs kuchukua timu?


    “Dakika ishirini baada ya Moyes kuondoka tulikuwa juu ya baiskeli zetu tukipasha misuli moto na mwenzetu mmoja akasema {Mnajua nini?Tumvae Giggs.Tunapaswa kumvaa na kumwambia aturudishie chips zetu.


    Pia katika kitabu hicho Ferdinand amemsifia Alex Ferguson kuwa ni kocha bora zaidi kuwahi kumfundisha.Amesema “Ferguson  alikuwa ni  kocha  muungwana mno hata kuwaomba msamaha wachezaji wake pindi alipowakosea.Ni kocha anayejua kupata kile anachokihitaji toka kwa mchezaji wake”.Tofauti na Moyes ambaye alileta mbinu za timu ndogo kwenye timu kubwa.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: FERDINAND:CHIPS ZILIMUONDOA MOYES UNITED Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top