728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, September 04, 2014

    USIJALI LOGA HATA ANGEKUA FERGUSON YANGEMKUTA TU


    MAKALA YA LEO

    Na. ALLEN KAIJAGE aka middle ya juu
                         0655106767
                         kaijagejr@gmail.com



                             
                  Ukitaka kuona maajabu jaribu kuthubutu kutembelea Tanzania.Kuna vitu vya ajabu ambavyo bila shaka vitakushangaza.Najua utafikiria kuhusu mlima Kilimanjaro na baadhi ya hifadhi za taifa kama Serengeti,manyara na mikumi.Lakini  milima mikubwa na mbuga za wanyama  hazipatikani Tanzania pekee,kuna nchi nyingi zinamiliki mbuga na milima mikubwa.Lakini kuna vitu vya pekee vinapatikana Tanzania tu na hutothubutu kuvisikia nchi nyingine.


                 Achana na madini ya tanzanite ambayo yanapatikana Tanzania pekee pia kuna aina ya watu wanapatikana Tanzania tu.Ni Tanzania tu mtu mwenye shahada ya ualimu anafanya kazi ya udaktari,mtu mwenye shahada ya sheria anafanya kazi ya usanifu majengo na mtu mwenye shahada ya uhasibu anafanya kazi ya uhandisi.Alafu tunategemea vitu bora kutoka kwa watu hao.Hiyo ndio Tanzania yangu.Kila sekta kuna watu wajanja wajanja ambao wana maneno mazuri ya ushawishi lakini ni wababaishaji.Kwenye sekta ya afya ndio hao wanaopasua watu vichwa badala ya miguu,kwenye sekta ya ujenzi ndio hao wanaojenga ghorofa leo keshokutwa linaanguka na kwenye michezo ndio hao wanaorudisha michezo yetu nyuma kwa kufanya kazi ambazo aziwahusu kwa manufaa yao.

                 Huku kwenye michezo ndio kunaongoza kwa makanjanja.Hawa wengi ni viongozi wajanja wajanja wanaofanya ujasiriamali kwenye michezo yetu.Kiongozi amepewa dhamana ya kuwa katibu lakini anataka kuingilia na kazi ya kocha,hapa unafikiri kocha atakuwa na sauti gani kama bosi wake ameamua kuingilia kazi yake?.Je unafikiri kocha huyo atafanya kazi yake kwa usahihi kama maamuzi ya kazi yake anafanyiwa na katibu wake?.Wana uchumi wanaamini ili upate uzalishaji mkubwa lazima ufanye kitu kinaitwa Division of labour(mgawanyo wa kazi) ila viongozi wa michezo yetu hususani mpira wa miguu hawataki kufuata sheria hiyo ya wachumi kwa kulinda matumbo yao

                Wakati napata habari za kufukuzwa kwa kocha logarusic wala sikustushwa.Kwani hiyo ni kawaida kwa timu zetu.Labda ningekua sio mtanzania hapo ndipo ningeshangaa kwa kocha aliyeongezewa mkataba anafukuzwa kabla hata ligi kuanza.Sawa kocha anaweza kuwa na matatizo lakini viongozi wa simba watakua na matatizo zaidi.Kocha loga kabla ya kutimuliwa kuna mahitaji aliwasilisha kwa viongozi kabla ya kuondoka lakini mahitaji yake hayakutimizwa.Kocha anahitaji kipa mrefu analetewa kipa ambaye hamuhitaji unafikiri hapo kuna nini kama si ukanjanja wa viongozi wa simba.
               Tatizo la viongozi wetu hawa ni ujuha wao wa matatizo ya ufundi kuliko kocha.Kila kiongozi akiona mchezaji anamvutia machoni mwake hulazimisha kusajiliwa hata kama si chaguo la kocha.Nani kawaambia mpira wa kisasa unaendeshwa hivo?. Mpira wa kisasa hauendeshwi kwa faida  ya mtu binafsi.Tatizo la simba si kocha bali ni viongozi.Makocha wangapi wanakuja na kuondoka?.Hao wakina phiri na milovan ambao ni vipenzi vya mashabiki wa simba walishawai kuja na kuondoka zaidi ya mara moja.Mashabiki wa simba kama mngepata nafasi ya kuwauliza sababu za kuondoka kwa makocha hao vipenzi vyenu bila shaka wangewaambia ni viongozi tu.Kwa simba wasipobadilisha mfumo wao wa madaraka hata aje sir alex ferguson au arsene wenger watatimuliwa tu.Kocha inabidi apewe nafasi ya kutoa maamuzi yote yahusiyanayo na mambo ya kiufundi.Kocha inabidi apewe nafasi ya kusajili wachezaji anaowataka  bila kusahau kupanga wachezaji anaowataka kwenye mechi husika.Maamuzi ya kocha inabidi yaheshimiwe na watu wote ikiwamo viongozi.Kocha mkishampa dhamana inabidi mumpe


    uhuru wa kufanya kazi yake sambamba na kumtimizia mahitaji yake ili pindi anapokosea muwe na nguvu ya kumhukumu.
                Timu zetu haziwezi kukaa na kocha hata miaka mitatu tu kwasababu ya matatizo ya viongozi wetu.Kocha kama ferguson amekaa miaka mingi Manchester united kwasababu ya viongozi bora aliowakuta ndani ya timu.ferguson angekua simba au yanga angeshasahaulika zamani kwenye ramani ya soka lakini mpaka sasa ni mtu na heshima zake kwenye jiji la Manchester.Viongozi walimpa kila kitu anachohitaji pia wakamuamini na kumvumilia na mpaka sasa ukizungumza kuhusu manchester united lazima umtaje sir alex.Ulishawai kujiuliza kama Manchester united wangemtimua sir alex baada ndani ya miaka minne ya mwanzo ambayo alikaa bila kombe lolote je Manchester united ingekuwa kama ilivyo sasa?.Kwangu mimi jibu ni hapana ila sitaki kuishi ndani ya ubongo wako na kuhisi jibu lako.
               Wapo makocha wengine wengi waliokaa kwa muda zaidi ya miaka 10 kwenye timu zao kama arsene wenger,sam allardyce na wengine wengi,Makocha hao wamekaa miaka mingi kwenye vilabu vyao kutokana na uongozi imara wa vilabu husika.Lakini kwa viongozi wetu wenye siasa nyingi na akili nyingi  za kutunisha matumbo yao kupitia timu zetu tutaendelea kufukuza makocha kila iitwapo leo.Muda mwingine huwa nawalaumu sana hawa wanachama wa vilabu vyetu kwa kurudisha miaka nyuma.Kila siku wanawapa dhamana watu wale wale na watu hao hufanya mambo yale yale ya kuendelea kudumaza vilabu husika.Kwa msisitizo kabisa nawaambia wanachama hao matatizo ndani ya timu zenu haziletwi na makocha bali viongozi wenu mnaowachagua kila siku.Loga usihuzunike kufukuzwa,hii ndio Tanzania na maajabu yake hata ferguson akija kufundisha vilabu vyetu watamtimua tu.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: USIJALI LOGA HATA ANGEKUA FERGUSON YANGEMKUTA TU Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top