728x90 AdSpace

  • Latest News

    Sunday, September 21, 2014

    UNITED KUMRUDISHA FALCAO MONACO IKIWA TU!!….



    Kutoka gazeti la Independent la leo jumapili habari zinasema moja kati ya kipengere ambacho hakikuwa kimewekwa wazi na klabu ya Manchester United juu ya usajili wa mshambuliaji hatari raia wa Colombia Radamel Falcao Garcia Zarate ni kwamba United haitasita kumrudisha haraka  nyota huyo katika klabu yake  mama ya Monaco ikiwa tu ataumia tena goti lake.



    Falcao ambaye mapema mwaka huu aliumia goti na kukaa nje kwa miezi sita (6) na kupelekea kuikosa michuano ya kombe la dunia nchini Brazil inasemekana kuwa mbali ya gharama zake za uhamisho wa mkopo kuwa juu pia kiwango cha mshahara alioukitaka ni sababu nyingine iliyoifanya Manchester United kuweka masharti magumu katika mkataba wa nyota huyo mwenye jicho la goli. 


    Hivyo basi uwepo wa Falcao Manchester United mbali ya kutegemea sana kiwango kizuri kitakacho ambatana na mvua ya magoli pia suala la afya ni jambo jingine kubwa litakalo mfanya nyota huyo aendelee kubaki Old Traford na hatimaye kupata mkataba wa kudumu wakati wa majira yajayo ya kiangazi.

    Je,Falcao ataepuka jinamizi la majeruhi na kubaki Old Traford?ni jambo la kusubiri na kuona....
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: UNITED KUMRUDISHA FALCAO MONACO IKIWA TU!!…. Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top