728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, September 09, 2014

    JOEL CAMPBELL:CAZORLA BALAA TUPU!!



    Habari na Paul Manjale

    Nyota kinda wa klabu ya Arsenal Mcosta Rica Joel Campbell ameshangazwa na uwezo wa nyota mwenzie katika klabu hiyo Muhispania Santi Cazorla na kusema ajabu ajabu!!


    Campbell akifanya mahojiano na mtandao wa klabu hiyo uitwao Arsenal Player alisema “Cazorla anashangaza sana,anafanya nijiulize mara mbilimbili yeye ni mchezaji wa aina gani? nadhani ni aina ya peke yake”


    “Lazima nikiri Cazorla ni mchezaji wa aina yake.Anaweza kupiga kona ama faulo sawa sawa kwa miguu yote bila kuonyesha tofauti yoyote ile.Anachokifanya kwa mguu wa kulia ndicho anachokifanya kwa mguu wa kushoto.Hicho siyo kitu cha kawaida kukiona ananishangaza kwakweli.”


    Akiulizwa kuhusu ushindani wa namba uliopo katika kikosi hicho hasa sehemu ya ushambuliaji  Campbell alisema “ Nadhani kila mchezaji atakuwa sambamba kugombea nafasi kikosi cha kwanza.Mshindani wangu mkubwa ni mimi nahitaji kufanya bidii mazoezini kila siku ili niweze kuwa bora zaidi.Ni heshima kuwa hapa leo”


    “Nadhani  ninaweza kuongeza kitu kikosini mfano kasi,magoli hata uwezo wa kukokota mipira.Mimi ni mchezaji mwenye uwezo wa kucheza kulia,kushoto ama kati kama mshambuliaji pekee”.

    “Ni jukumu la mwalimu kunipanga sehemu anayoona ninahitajika zaidi na nitajitahidi kufanya vizuri. ” Alimaliza Campbell shujaa wa Costa Rica katika fainali zilizoisha za kombe la dunia nchini Brazil.



    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: JOEL CAMPBELL:CAZORLA BALAA TUPU!! Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top