728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, September 25, 2014

    CHELSEA,ARSENAL ZAMFUKUZIA COURTOIS MPYA



    Vilabu vya jiji la London Chelsea na Arsenal vimeingia katika vita kali ya kumtaka mlinda mlango kinda raia wa Ubelgiji Mile Svilar (15) ambaye anafananishwa na mlinda mlango namba moja wa klabu ya Chelsea Thibaut Courtois.


    Inasemekana klabu ya Arsenal tayari imeshampa  kinda huyo  mwaliko wa kutua Emirates kwa ajili ya majaribio ya siku kadhaa.Klabu ya Chelsea yenyewe tayari imeripotiwa kukamilisha zoezi hilo mapema.Wakati huohuo klabu ya Manchester United nayo imeripotiwa kumuulizia  kinda huyo.


    Lakini baba mzazi wa kinda huyo,Ratko Svilar ambaye ni mlinda mlango wa zamani wa klabu ya Antwerp amesema ofa yoyote toka vilabu vya England haitasikilizwa kwa wakati huu na badala yake itapuuzwa kutokana na kuwa tayari wana makubaliano na klabu ya Anderletch.


    Amesema “Mile ameshafanya majaribio na Chelsea,Manchester United wameshaanza kumuulizia.Kila mtu anamtaka,lakini tayari tuna makubaliano na Anderletch japo hatoweza kusaini mkataba mpaka atakapofikisha miaka 16.Sidhani kama kuna  sehemu nzuri kwake kwa sasa zaidi ya Anderletch”

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: CHELSEA,ARSENAL ZAMFUKUZIA COURTOIS MPYA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top