728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, September 19, 2014

    GUTIERREZ:RAFU YA SAGNA IMENISABABISHIA KANSA



    Habari na Paul Manjale
     
    Unamkumbuka yule  winga  mrefu wa klabu ya Newcastle United,Yule aliyekuwa na nywele ndefu na nzuri kama za akina Rihanna na Beyonce?Hapa namuongelea Jonas Gutierrez Je,ukimuona leo utamtambua?unajua aliko,anachezea klabu gani kwa sasa?
    Gutierrez anavyoonekana sasa


    Haya ni baadhi tu ya maswali ambayo unaweza ukajiuliza kwa haraka haraka na usipate majibu ya uhakika juu ya nyota huyu wa soka.Nani alimjua kabla ya kutua Newcastle misimu kadhaa nyuma,nani anayejua aliko?Siyo maarufu sana kama akina Messi,Di Maria ama Aguero lakini kwa sasa anaweza akawa na kitu ambacho mimi na wewe tungependa kukifahamu.


    Gutierrez huyu wa sasa siyo Yule tunayemfahamu,siyo Yule tuliyezoea kumuona kila wikendi  akiwa na jezi za rangi ya punda milia akisukuma gozi la ng’ombe pale katika dimba la St.James Park na madimba mengine England.Gutierrez wa sasa ni mgonjwa,hawezi tena kufanya zile vurugu zake uwanjani,hawezi tena kukimbia kwa ile kasi tuijuayo….Gutierrez anaumwa Kansa.Soka ndiyo basi tena anaungana na nyota kama Jason Cundy (1997 aligundulika kuwa na kansa),Alan Stubbs (1999),John Hartson (2009) na Stiliyan Petrov (2012).

    Jonas Guttierrez amefichua kuwa mgongano kati yake na aliyekuwa mlinzi wa kulia wa klabu ya Arsenal Mfaransa Bacary Sagna ulifanya afanyiwe vipimo ambavyo ilikuja kugundulika kuwa nyota huyo ana Kansa.


    Nyota huyo wa zamani wa Newcastle amekuwa akipambana na ugonjwa huo kwa mwaka mmoja sasa hata kupelekea kuondolewa kwa korodani/kende yake ya kushoto mwezi Octoba mwaka jana.Gutierrez ambaye kwa sasa ana umri wa miaka 31 aliyasema hayo jumanne wiki hii wakati akifanya mahojiano na chombo kimoja cha habari kiitwacho TYC Sports cha nyumbani kwao Argentina.

    Alisema “Ilikuwa ni Mei 2013,niligongana vibaya na Sagna nikaumia maeneo ya viungo vya uzazi.Tangu hapo nikawa na maumivu makali mno ambayo hayakuisha.Niliongea na Daktari mara moja na akaniambia usijali yatapoa tu.
    Gutierrez akigugumia kwa maumivu baada ya kugongana na Sagna


    “Hali ilijirudia tena wakati wa likizo na nikajisikia maumivu  sana sehemu ya korodani.Kuna wakati korodani zilichachamaa mpaka nikawa nashindwa kuvaa nguo za ndani.Nilirudi kwa daktari  na kumsimulia kila kitu,akanishauri nifanye vipimo vya Ultrasound ambayo vilikuja kugundua kuwa nina uvimbe/mtutuko na nilipaswa kufanyiwa upasuaji mapema”

    Baada ya kuambiwa nijiandae kwa upasuaji niliondoka nikilia na kurejea nyumbani na kumwambia yote baba yangu aliyekuwa amekuja kunitembelea.Niliongea na uongozi wa klabu juu ya tatizo langu na nia yangu ya kutaka kwenda kutibiwa nyumbani Argentina, nikaruhusiwa.

    Gutierrez alirudi England katika klabu yake ya Newcaste baada ya upasuaji na kukutana na balaa toka kwa kocha wake Alan Pardew….anasema 

    “Niliporejea kikosini mwishoni mwa Novemba kuendelea na utaratibu wa mazoezi,timu ilikuwa vizuri lakini katikati ya mwezi wa Desemba kocha Pardew aliniambia huna nafasi tena kikosini na badala yake tafuta timu ukacheze kwa mkopo.Nilishangazwa sana na uamuzi ule ukizingatia nimekuwa nikicheza karibu kila siku kwa kipindi chote cha miaka mitano ambacho nimekuwa hapa,sasa iweje wanitoe kwa mkopo?iliniuma sana.Sikuwa na jinsi nikaenda Norwich City kwa mkopo mwezi januari.

    Je,vipi bado una mkataba na Newcastle na vipi kuhusu gharama za matibabu unalipia wewe au wao?

    Gutierrezi “Ndiyo bado nina mkataba nao ambao unaisha msimu huu,najilipia mwenyewe matibabu,pesa siyo kitu muhimu zaidi.Kitu muhimu ni uzima.

    Huna korodani/kende moja je vipi wazazi wakihitaji wajukuu?

    Gutierrezi “Unapokuwa na tatizo kama hili wanakupeleka kwenye benki ya kuhifadhia mbegu za kiume na unaacha sample kadhaa za mbegu hapo kama tahadhari ikiwa kende nyingine itaharibika.Lakini naamini kwamba nyingine iko vizuri hakuna kitakacho haribika”

    Sasa kwanini umechelewa kuupasha habari umma kuhusu ugonjwa wako na hata useme sasa?

    Gutierrezi “Ni jambo binafsi sana lakini juzi nilipata email(barua pepe) kuhusu mwigizaji mmoja wa kike ambaye nae ana pambana na tatizo kama langu na alikuwa akionyesha picha zake hadharani za wakati akiwa na nywele zake na alipoanza kupoteza nywele na yote aliyokuwa akiyapitia.Nikaona na mimi napaswa kusema ili watu wajue na labda inaweza kuwa ni msaada kwa wengine”


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: GUTIERREZ:RAFU YA SAGNA IMENISABABISHIA KANSA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top