728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, September 06, 2014

    BRAZIL YAIFUNGA COLOMBIA,NEYMAR SHUJAA




    Timu ya taifa ya Brazil imepata ushindi wake wa kwanza tangu  kuondolewa kwa aibu ya kubugizwa goli 7-0 na Ujerumani  katika mchezo wa nusu fainali wa kombe la dunia zilizofanyika nchini kwao miezi miwili iliyopita baada ya alfajiri ya leo kuibuka na ushindi wa goli 1-0  dhidi ya timu ya taifa ya Colombia katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki.
    Neymar akishangilia goli dhidi ya Colombia


    Huu unakuwa ni mchezo wa pili kwa miamba hiyo kukutana ikiwa imepita miezi miwili na siku kadhaa tangu timu ya taifa ya Brazil ilipofanikiwa kuwafunga na kuitoa Colombia kwa goli 2-1 katika mchezo wa robo wa kombe la dunia uliopigwa katika dimba la Fortaleza ambayo nyota wa Brazil Neymar alichezewa rafu iliyopelekea nyota huyo kuvunjika mfupa wa mgongo.
    Neymar akiwania mpira na mlinzi wa Colombia Zuniga



    Brazil iliyokuwa chini ya kocha mpya Carlos Dunga na nahodha mpya Neymar Dos Santos ilijipatia goli lake la ushindi na la pekee kupitia Neymar  dakika ya 83 kwa mkwaju wa adhabu uliomshinda mlinda mlango David Ospina na kuamsha ndelemo hoi hoi na vifijo kutoka wa mashabiki wa timu hiyo waliojitokeza kwenye uwanja wa Sun Life,Miami (Marekani) uliokuwa na jumla ya watazamaji 73,429. 
    Falcao akigombea mpira na walinzi wa Brazil Luiz na Maicon


    Katika mchezo huo uliochezeshwa na mwamuzi Dave Gantar ilishudiwa mwamuzi huyo akipata wakati mgumu kutokana wachezaji wa timu zote mbili kuchezeana rafu mara kwa mara kulikopelekea  kutolewa kwa jumla ya kadi saba za njano kutolewa huku winga wa Colombia Juan Quadrado akitolewa uwanjani baada ya kuonyeshwa kadi mbili za njano kufuatia kumchezea rafu  Neymar katika matukio mawili tofauti.
    Cuadrado na Felipe Luiz wakigombea mpira


    Huu unakuwa ni mchezo wa 61 wa kocha Dunga akipata ushindi katika michezo 43 akitoka sare  12 na kufungwa  6 pekee ndani awamu mbili alizofundisha akiwa kama kocha mkuu wa timu hiyo.Dunga ambaye amerithi mikoba ya kocha aliyetimuliwa Felipe Scolari aliita wachezaji kumi tu waliokuwepo katika fainali za dunia huku wanne pekee wakianza katika kikosi chake cha  kwanza.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: BRAZIL YAIFUNGA COLOMBIA,NEYMAR SHUJAA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top