728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, September 08, 2014

    ROONEY:STERLING KAMA OVERMARS

    Habari na Paul Manjale



    Mshambuliaji na nahodha wa klabu ya Manchester United na timu ya taifa ya England Wayne Rooney amemfananisha winga kinda wa nchi hiyo Raheem Sterling na winga nguri wa zamani wa klabu ya Arsenal na timu ya taifa ya Uhoranzi Marc Overmars.



    Rooney akifanya mahojiano kabla ya mchezo wa leo wa kusaka tiketi ya kushiriki michuano ijayo ya Ulaya (Euro 2016)  dhidi ya timu ya taifa ya Uswisi.


     Alisema “Nilikaa nae chini kabla ya kombe la dunia nikamwonyesha video za Marc Overmars kwasababu ananikumbusha mno vitu vya mkongwe yule”



    “Nafikiri ana uwezo wa kuwa bora zaidi kama alivyokuwa Overmars.Bado ni mdongo lakini uwezo anaounyesha ni wa ajabu sana”.


    “Ni mchezaji mzuri sana.Hili lilijionyesha msimu uliopita na hata mwanzo wa msimu huu”


    “Ni mchezaji mzuri anaweza kucheza mbele kabisa  ama pembeni.Japo ana umbile dogo lakini ni mjanja, imara na ana nguvu sana”



    “Atakuwa ni mchezaji muhimu sana kwa kipindi cha miaka 10 au 15 kwa England na na bahati mbaya kwa klabu yake ya Liverpool”.Alimaliza Rooney ambaye leo atakuwa na kibarua kigumu cha kukiongoza kikosi cha England kupata pointi tatu muhimu mbele ya wenyeji Uswisi.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: ROONEY:STERLING KAMA OVERMARS Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top