728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, September 05, 2014

    WENGER NA AZIMIO LA ARUSHA



         MAKALA YA LEO    

         Allen kaijage
         0655106767
         kaijagejr@gmail.com

       

                                                    
    Azimio la Arusha si neno geni kwa Watanzania.Wengi wao tumelisikia kama hatukusoma sehemu,Pia wachache kati yetu walikuwepo kipindi cha azimio la Arusha.Azimio la Arusha ni tamko rasmi la kisiasa lililokusudiwa kuingoza nchi yetu katika misingi ya ujamaa.Azimio hili lilipitishwa jijini Arusha chini ya uongozi wa baba wa taifa hayati mwalimu Julius K.Nyerere mnamo mwaka 1967. Lengo kuu la azimio la Arusha ilikua ni kupunguza au kuondoa unyonyaji na uonevu wa mabepari.Kwa hekima za mwalimu nyerere akaona sera ya ujamaa na kujitegemea ndo utakuwa mwarobaini kwa mabeberu na kuleta ustawi ndani ya nchi.


    Mwalimu alikua na imani kubwa na ujamaa haswa baada ya mwaka mmoja nyuma kabla ya azimio hilo kwenda kumtembelea mjamaa mao aliyekua kiongozi wa china. Nyerere aliamua kuamishia madesa yake ya ujamaa nchini akiwa na matumaini na malengo mazuri juu ya nchi yetu  kupitia ujamaa ingawa hakufanikiwa.Kambona na profesa babu waliona mbali na kumshauri aachane na misingi ya mfumo wa ujamaa ili kunusuru viwanda lakini Nyerere aliweka pamba masikioni.
    Uzalishaji ulipungua kwa kiasi kikubwa uliopelekea wananchi kuikatia tamaa sera ya ujamaa.Labda ni kwasababu ya Vita ya Uganda au anguko la bei ya bidhaa zetu ama tatizo la kimataifa la mafuta miaka ya mwanzoni mwa 1970.Hizo zote zinaweza kuwa sababu ya kufeli kwa ujamaa.Mwalimu kwa busara zake ilipofika mwaka 1985 akatangaza kutogombea tena urais na kumwachia rais mwinyi  aliyeingia nchini na taratibu za soko huria na huo ndio ukawa mwanzo wa kufa kwa ujamaa.
                Soko huria (Open market  )ndio mfumo unaoendesha dunia ya sasa.Soko huria imefungua milango kwa wafanyabiashara kuuza au kununua bidhaa kokote wapatapo soko.Wana uchumi wanasema kuwa katika dunia ya sasa hakuna nchi ambayo ni wajamaa tu(pure socialist) wala mabepari tu(pure capitalist) zaidi ya nchi nyingi kuchanganganya ubepari na ujamaa(mixed economy).Huku misingi ya ubepari ikilenga ushindani wa kibiashara wakati ujamaa ukilinda utu.Hapo utaona Dunia kwa ujumla imeruhusu ushindani huru wa kibiashara kwa misingi isiyo ya unyonyaji.Utapata zaidi ya utakavyozalisha.Utapata kiasi cha jasho lako huku lazima ukubali kuliwa ili ule.

    Sera hii inatawala sekta zote duniani.Hata sekta ya michezo pia inahitaji uwekezaji wa hali ya juu kufikia mafanikio.Ndio maana nchi zilizofanikiwa sana kwenye michezo hasa soka ni zile zilizowekeza zaidi kwenye mchezo huo.Hata vilabu vilivyofanikiwa Duniani ni vile vilivyowekeza zaidi kwa wachezaji.Lakini bado kuna watu wabishi wanaoamini ujamaa katika soka .Wapo  macommunist wanaofikiri watafanikiwa kwa sera zao za kale.Wapo macomunist wengi lakini leo ntamzungumzia mmoja.

    Huyu wanamuita Arsene wenger.Muumini wa azimio la Arusha.Mcomunist asiyekubali kushindwa,hataki mabadiliko wala kubadilishwa.Huendelea kuamini kwenye kile anachokiamini hata kama hakina manufaa.Mwalimu wenger kwa arsenal ni kama mwalimu Nyerere kwa Tanzania,Kama Nyerere alivyoleta uhuru kwa Tanganyika ndivyo hivyo wenger alivyopigania uhuru wa arsenal na kuirudisha kwenye chati baada ya kupotea kwa muda.Tofauti  yao ni kuwa Mwalimu Nyerere maji yalipozidi unga aliamua kujiweka kando lakini Wenger bado anakomaa na upishi huku kila siku akipika ugali wa mabuja kwa ubahiri wa kununua unga.Wenger msimu uliopita wa ligi kuu England alikutana na 

    maswahiba mazito kutoka kwa Chelsea,City na Liverpool lakini bado wenger ni Yule Yule asiyetaka kujifunza kutoka kwenye majanga yaliyomsibu.

    Ukiangalia kikosi cha Arsenal utaona mapungufu kwenye nafasi ya ushambuliaji bila kusahau nafasi ya kiungo mkabaji.Lakini wenger bado amefumbia macho swala hili na kuendeleza sera zake za ujamaa akiamini ujio wa welbeck akisaidiana na sanogo watafunga magoli mengi huku akisahau mabepari City wana Aguero,Dzeko na Djovetic ,Chelsea wana  Costa,Drogba n a Remmy.Huku mabepari hayo yakiwa na viungo wakabaji wa nguvu kama Fernandinho na Fernando kwa upande wa city,Matic na mikel kwa upande wa Chelsea yeye mcomunist ana wazee  arteta na flamin ambao wote damu zimeshachoka.

    Hapo mjamaa wenger kila siku  ataendelea kulalamika kuhusu vitendo vya unyanyasaji  na  uonevu anavyofanyiwa mabepari wa City na Chelsea ilihali ana uwezo wa kubadilisha mawazo yake ya ujamaa na kuingia moja kwa moja kwenye Dunia ya ushindani kuwakabili mabeberu hayo.Wenger amejua kuiga mfumo wa uchezaji wa Barcelona ila ameshindwa kugundua Barcelona pia wameachana na sera ya ujamaa na kuingia kwenye mixed economy (kuchanganya ubepari na ujamaa) ndio maana utaona Barcelona ya sasa inatumia bajeti ya usajili wa wachezaji wote wa arsenal kumnunua luis suarez na  kuacha utamaduni wao wa kuwaamini wakina Tello na Bojan.

    Dawa ya moto ni moto.Dawa ya bepari ni bepari na beberu ni beberu.Wenger kama anataka kuondoa aibu ya vipigo vya magoli mengi anavyovipata kutoka kwa city na Chelsea na kukabiliana nao jino kwa jino inabidi aachane na misingi ya azimio la Arusha na kuvaa roho ya ubeberu.Asikwambie mtu Arsenal haiwezi kushindana na City na Chelsea,Arsenal ni timu tajiri kuliko City na Chelsea tofauti yao inakuja kwenye sera ya usajili ya klabu.

    Wenger ni mmoja wa makocha walioachwa huru na vilabu vyao kuhusu swala la usajili.Yeye ndie muamuzi juu ya mambo yote ya kiufundi.Lakini wenger  anautumia uhuru wake kuyaishi maisha ya kale ya ujamaa.Ndio maana anaishi kwenye kile alichokiamini ingawa kimemdumaza yeye na timu kwa ujumla.Hataki kukubali kuwa mpira sasa umebadilika ndio maana hataki kubadilika ingawa anaona mbinu zake zinafeli.Kwa manufaa ya arenal wenger inabidi afanye kati ya hivi viwili,Aachane na sera zake za zamani ambazo mimi nazifananisha na azimio la Arusha na sera ya ujamaa na aingie kwenye soko la ushindani ili kukabiliana vilivo na mabepari Madrid,Barca,City na Chelsea kama anataka kuirudisha Arsernal ya ushindani,Ama wenger inabidi afanye alichokifanya Mwalimu Nyerere baada ya kuona ujamaa unaelekea kumlipua akaaamua kukaa kando,Pia wenger kwa busara kama za Mwalimu angekaa kando kupisha Makocha wa kisasa waendeleze mapambano yaliyomshinda.

                                                                                

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: WENGER NA AZIMIO LA ARUSHA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top