728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, September 23, 2014

    DIABY DIMBANI LEO KUIVAA SOUTHAMPTON CAPITAL ONE CUP



    Baada ya kuwa nje kwa kipindi kirefu kutokana na majeraha ya mara kwa mara hatimaye kiungo Abou Diaby anarejea leo dimbani kuichezea klabu yake ya Arsenal katika mchezo wa kombe la Capital One dhidi ya klabu ngumu ya Southampton.Diaby amekuwa nje ya dimba kwa kipindi cha siku 556 tangu alipoumia Machi 2013 katika mchezo dhidi ya Swansea.


    Akielezea kurejea huko kwa kiungo wake kocha Arsene Wenger amesema “Diaby alicheza dakika 90 wiki iliyopita katika mchezo uliovikutanisha vikosi Arsenal na Aston Villa vya wachezaji waliochini ya miaka 21 (U21) hivyo atakuwepo katika mchezo wa jumanne dhidi ya Southampton”.


    “Yuko vizuri kiafya na kiakili mara zote amekuwa akirejea dimbani licha ya kukumbwa na majeraha,ni mtu anayejitolea kwa ajili ya timu hivyo mchango wake unahitaji kuheshimiwa.Mimi ni muumini mkubwa wa soka yake lakini nasikitika kwakuwa ameshindwa kuionyesha kutokana na kuumia umia”


    Mbali ya Diaby pia kocha Wenger amepanga kuwapa nafasi makinda na wachezaji wanaokosa namba kikosi cha kwanza katika mchezo huo huku akiwaapumzisha wachezaji wake wengi wazoefu kwa ajili ya mchezo wa wikendi hii dhidi ya mahasimu wao Tottenham hotspurs.Baadhi ya makinda watakaocheza leo ni Hector Bellerin,Isack Hyden,Chuba Akpom,Semi Ajayi watakaosaidiana na wazoefu Joel Campbell,David Ospina pamoja na Lukas Podolski.


    Michezo mingine ya Capital One ikiwa ni roundi ya tatu ni kama ifuatavyo


    Liverpool vs Middlesbrough
    Swansea vs Everton
    Sunderland vs Stoke
    Mk Dons vs Bradford

    Kesho jumatano ni tarehe 24
    Chelsea vs Bolton
    Crystal palace vs Newcastle
    Man City vs Sheff Wed
    West Brom vs Hull



    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: DIABY DIMBANI LEO KUIVAA SOUTHAMPTON CAPITAL ONE CUP Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top