728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, September 29, 2014

    CHELSEA KUHAMA DARAJANI,KUDHAMINIWA NA WATURUKI



    Klabu ya Chelsea  huenda ikauhama kwa muda uwanja wake wa Stamford Blidge maarufu kama darajani na kuhamia uwanja wa Twickenham.Habari za kuaminika zinasema klabu hiyo iko katika mazungumzo mazito ya kuomba kuutumia uwanja huo kwa msimu mmoja wa 2016/17,Twickenham ni uwanja maarufu sana kwa mchezo wa rugby jijini London na haujawahi kutumiwa kwa soka tangu kujengwa kwake. 
    Twickenham kwa nje



     
    Ikiwa ombi hilo litafanikiwa Chelsea itautumia uwanjao huo kwa mechi zake za nyumbani na hivyo kutoa nafasi kwa uwanja wa Stamford Blidge kufanyiwa upanuzi toka idadi ya sasa ya watazamaji 41,800 mpaka 60,000 na hivyo kuifanya miamba hiyo kuwa na msuli wa kuchuana kiuchumi na vilabu vingine vikubwa Ulaya kama Manchester United,Arsenal,Bayern Munich,Barcelona na Real Madrid.
    Kwa ndani


    Hili litakuwa ni jaribio la pili la mmiliki wa klabu ya Chelsea kuwa na mipango kama hiyo baada ya mara ya kwanza kufanya mipango iliyokuja kushindikana ya kuhamia Battersea Power Station kusini mashariki mwa London.


    NB;Stamford Blidge  ulianza kutumiaka mwaka 1876 mpaka sasa umeshafanyiwa upanuzi mara mbili na ni uwanja wa nane (8) kwa ukubwa kati ya viwanja vinavyotumiwa kwa mechi za ligi kuu.

    Wakati huo huo kampuni ya Kituruki ya safari za anga ya Turkish Airline imetangaza kupitia mtandao wake kuwa imefikia makubaliano ya kuidhamini klabu ya Chelsea.Nembo ya Turkish Airline itaanza kuonekana katika jezi na bidhaa nyingine za klabu hiyo msimu ujao (2015-2016) na kuhitimisha safari ndefu iliyokuwa na mafanikio na kampuni ya Samsung toka mwaka 2005-2015.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: CHELSEA KUHAMA DARAJANI,KUDHAMINIWA NA WATURUKI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top