728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, September 11, 2014

    MOURINHO:GURDIOLA ANATOKA KIPARA KWA KUWA HAENJOY SOKA




    Kocha mwenye tambo na maneno mengi Mreno Jose Mourinho ameibuka na kudai kuwa kocha wa klabu ya Bayern Munich Muhispania Pep Guardiola ananyonyoka nywele na kubaki kipara kwasababu haenjoy (hafurahii) mchezo wa soka kama yeye.




    Mourinho ameyatoa maneno hayo baada ya wawili hao  kuibua ubishani wakati wa mkutano wa makocha uliofanyika katika ofisi za makao makuu ya UEFA kujadili urefu wa nyasi viwanjani.Habari zinasema mzozo huo ulianza baada ya Guardiola kusisitiza kuwa urefu wa nyasi usizidi sentimeta 1.5 ili kuufanya mchezo uwe na kasi na mvuto.




    Kufuatia maoni hayo Mourinho alipinga na kusema “Kila mtu ana aina yake ya uchezaji,ambayo inapaswa kuheshimiwa.Soka inaweza ikawa  na mvuto kwa njia nyingi.

    Guardiola akajibu “Uzuri wa soka unategemea timu inafundishwa na kocha yupi.Inaonekana Mourinho anapendelea zaidi matokeo kuliko mvuto/uzuri.
                                                    
                                                        

    Baada ya maneno hayo Mourinho alijibu mapigo kwa kusema “Unapofurahia/enjoy kile unachokifanya huwezi kunyonyoka nywele na Guardiola ana uwalaza/upara ni kwasababu hafurahii soka.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MOURINHO:GURDIOLA ANATOKA KIPARA KWA KUWA HAENJOY SOKA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top