728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, September 18, 2014

    STEVE:CHUKI ZIMENIKIMBIZA YANGA



    Mbali ya mshambuliaji Mbrazil Geilson Santos ” Jaja”kutawala midomoni mwa mashabiki wa soka nchini baada ya kufunga goli mbili na kuiwezesha klabu yake ya Yanga kutwaa Ngao ya Jamii kwa jumla ya goli 3-0 dhidi ya klabu ya Azam katika mchezo uliopigwa katika uwanja wa taifa jumapili iliyopita jina jingine ambalo liingia kwa kasi midomoni mwa wapenda soka lilikuwa ni jina la shabiki maarufu Steven Charles maarufu kama Steve Yanga baada ya kutinga uwanjani hapo akiwa amevalia jezi ya Azam na kukaa mbali kabisa na jukwaa la klabu ya Yanga.
    Picha ya Steven iliyotibua hali ya hewa


    Mengi yameongelewa sana kuhusu kitendo cha shabiki huyo ambaye huenda ndiye shabiki maarufu zaidi wa mpira kuliko wote nchini Tanzania kwa miaka hii ya karibuni.Habari hizo ziliifikia timu makini ya MchakaMchaka Viwanjani na hatimaye ikaanza kufanya mawindo ya chini kwa chini kumsaka na kumtia mkononi shabiki huyo ili atueleze imekuwaje,Je ni mbwembwe tu kile tunachokisikia ama ndiyo hali ilivyo?
    Jumatatu asubuhi mwandishi wa habari hii alinyanyua simu na kumtafuta Steve na maongezi yalikuwa hivi..
    Steve akionyesha jeuri ya pesa


    Manjale:Mambo vipi Steve?

    Steve:Manjale najua unachotaka kuongea

    Manjale:Steve nasikia umeikimbia Yanga kaka imekuwaje?
    Steve akiongoza kikundi mjengoni kwetu house kucheza mziki


    Steve:Mwanjala (hapa akachapia jina langu) ni maisha tu kaka.

    Manjale:Steve naomba dakika chache tu unijibu maswali mawili matatu niliyonayo hapa.

    Steve:Kaka nina haraka kuna sehemu nawahi.(Simu ikakatwaa)

    Mwandishi hakukata tamaa Jumanne mchana akampigia tena simu lengo likiwa ni lile lile kuujua undani wa kile kinachoongeleka juu yake lakini simu iliishia kukatwa na kuingia ujumbe mfupi usemao “Kaka niko bize kidogo nafanya interview na BBC Swahili nitakutafuta baadae”.Nikasema poa kaka ila kuna kitu nataka tuongee.

    Mwandishi akiwa hana hili wale lile siku ya jumatano asubuhi saa 7:12 simu  yake iliita kutazama jina alikuwa ni Steve Yanga…….na maongezi yalikuwa hivi

    Manjale:Nikiwa nimekariri Mambo vipi Steve Yanga?

    Steve:Aah!!Manjale hilo jina silitaki kama huwezi kuniita Steve Azam basi ishia Steve.Vipi tunahitaji kuonana ana kwa ana ama hata kwa simu inatosha?

    Manjale:Ikabidi niwe mpole pale nikamwomba msamaha rafiki yangu huyu na michapo ikaendelea.

    Steve:Manjale vipi ni kipi hicho unachotaka kujua?afu ujue sifanyagi interview bure bure kaka ila kwasababu ni wewe tuendelee.

    Manjale:Eehe!!Kaka vipi hili la wewe kuhamia Azam ni kweli?

     Steve:Manjale ulichokisikia na kukiona  kwenye mitandao ni kweli kabisa mimi kwa sasa siyo shabiki wa Yanga tena nguvu na akili yote iko Azam Fc wazee wa mipango hai.

    Manjale:Duh makubwa!!Hebu kwanza rudi nyuma kidogo unipe historia yako fupi hasa ni lini ulianza kuishabikia Yanga?
                                                
    Steve:Kwa kusema ukweli (msishangae huyu jamaa katokea Mbeya kwa kuchapia jina langu) Mwanjala mimi nilianza kuishabikia Yanga mwaka 2008 na jina langu lilikuja kufahamika sana baada ya kulia pale uwanja wa taifa siku Yanga ilipofungwa goli 5-0 na Simba.Kabla ya hapo hakuna shabiki wa kiongozi wa Yanga aliyekuwa akinifahamu lakini baada ya picha zangu na clip kusambaa kwenye matelevisheni na mitandao mbalimbali ya kijamii nilianza kutwafutwa na kupongezwa kuwa mimi ni shabiki wa ukweli kabisa.

    Manjale:Aisee safi sana,Eeh vipi hebu tuambie nini kimekutoa Yanga na kukupeleka Azam?

    Steve:Manjale,baada ya mimi kutoka katika shindano la Kwetu House lililokuwa chini ya Azam Media ambalo hata wewe Manjale ulikuwepo,maisha kwangu yakawa magumu.Watu wakaanza kunisakama na kuniita msaliti eti kwanini nimeingia katika shindano hilo wakati Azam na Yanga hawapatani?Nikawa sina raha huyu anasema hiki Yule ansema kilebasi ikawa ni shida mtindo mmoja.Kwakweli nilikuwa naumia sana na kujiuliza maswali mengi kwanini hivi…….kosa langu ni lipi hapa?kwenda kwenye shindano hilo ndiyo iwe  tabu?

    Manjale:Aisee pole sana Steve….vipi ni sababu hiyo tu ama kuna nyingine?

    Steve:Sababu nyingine ni kwamba nimekuwa sina maelewano mazuri na baadhi ya viongozi wa Yanga kwani wamekuwa wakinitolea lugha chafu pindi ninapokuwa nikiwafuata kwa maswala mbalimbali mfano……. na …….(akawataja viongozi hao).Lakini napenda sana kumshukuru Mwenyekiti Yusuph Manji kwa zawadi ya bodaboda na cheti.

    Manjale:Hebu niambie Azam wanajua uwepo wako kama shabiki wao na ilikuwaje?

    Steve:Azam wanajua hilo na kabla sijafanya maamuzi hayo niliupigia simu uongozi na kuongea nao kirefu.Nashukuru wamenielewa na kunipokea kwa mikono wiwili.
    Manjale:Safi kaka,nasikia wanataka kukupa ajira pia?
    Mwandishi wa habari hii akiwa na waliokuwa washiriki wenzake aktika shindano la kwetu house

    Steve:Aah Manjale umepata wapi habari hizo?Ila ni kweli hiyo ishu ipo japo haijawa rasmi sana ikiwa tayari nitakwambia.
    Manjale:Basi poa Steve asante sana kwa ushirikiano wako
    Steve:Poa poa kaka panapo chochote tutafutane
    Manjale:Poa kaka tuko pamoja
    Huo ndiyo ukawa mwisho wa interview yetu,nadhani lile giza tulilokuwa nalo juu ya uamuzi wa huyu shabiki limeondoka na kila kitu kiko hadharani.
    Asante kwa kuwa pamoja nasi……………….”karibu kwa maoni yako”
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: STEVE:CHUKI ZIMENIKIMBIZA YANGA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top