728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, September 09, 2014

    ENGLAND YATAKATA EURO 2016,WELBECK WE ACHA TU!!



    Habari na Paul Manjale

    Timu ya taifa ya England imeanza vizuri kampeni yake ya kuisaka tiketi ya kushiriki michuano ijayo ya Ulaya (Euro 2016) baada ya kuibamiza timu ya taifa ya Uswisi kwa jumla ya mabao 2-0.
    Welbeck akishangilia goli la pili dhidi ya Uswisi


    England ilijipatia magoli yake kipindi cha pili cha mchezo huo wa kundi E uliopigwa katika dimba la St Jacob Park mjini Basel kupitia kwa mshambuliaji wake Danny Welbeck dakika za 59 na 90 akitumia vyema pasi za winga Raheem Sterling.
    Welbeck akifunga goli la kwanza


    Baada ya mchezo huo kocha mkuu wa timu ya taifa ya England Roy Hodgson aliwasifu wachezaji wake na kusema wameutendea haki mfumo wa 4-4-2 diamond huku pia akionyesha ishara ya dole gumba kwa viungo wake Jack Wilshere,Raheem Sterling na Fabian Delph na mlinzi John Stone kwa kuonyesha soka safi na kuifanya timu icheze kwa uelewano mkubwa.
    Kocha Hodgson akishangilia moja kati ya magoli dhidi ya Uswisi


    Huu ni mchezo wa kwanza kwa timu ya taifa ya Uswisi inayonolewa na kocha Vladimir Petkovic kupoteza ikiwa nyumbani baada ya kufanya hivyo miaka minne iliyopita kwa kufungwa na England  Oktoba mwaka 2010 kwa jumla ya magoli 3-1.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: ENGLAND YATAKATA EURO 2016,WELBECK WE ACHA TU!! Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top