728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, September 11, 2014

    THIBAUT COURTOIS ALAMBA MKATABA WA MIAKA 5 CHELSEA




    Habari na Paul Manjale

    Klabu ya Chelsea inaonekana kunogewa zaidi na huduma za mlinda mlango wake raia wa Ubelgiji Thibaut Courtois  (22)baada ya hivi punde kutangaza kuwa imemuongezea mkataba mpya wa miaka mitano nyota huyo.


    Taarifa kutoka klabu ya Chelsea imesema “Chelsea Football Klabu inayofuraha kutangaza kuwa Thibaut Courtois amesaini mkataba mpya wa miaka mitano leo hii”


    Courtois ambaye alisajiliwa klabuni hapo mwaka 2011 akitokea klabu ya nyumbani kwao  ya KRC Genk na kucheza kwa mkopo wa misimu mitatu katika klabu ya Atletico  Madrid ya Hispania na kutwaa taji la La Liga amerejea Stamford blidge msimu huu na kufanikiwa kumpora namba aliyekuwa mlinda mlango namba moja wa klabu hiyo kwa muda mrefu Peter Cech (32).


    Baada ya kusaini mkataba huu Courtois alikuwa na haya ya kusema “Nimefurahi kusaini  mkataba huu mpya wa miaka mitano.Ni furaha pia kujua kuwa nitaendelea kuwa hapa kwa kipindi kingine kirefu,kilichopo akilini mwangu kwa sasa ni kuendelea kuipigania timu hii.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: THIBAUT COURTOIS ALAMBA MKATABA WA MIAKA 5 CHELSEA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top