728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, September 24, 2014

    DHAMBI YA GUARDIOLA DARASA KWA SOKA LA BONGO



                                                        MAKALA YA LEO
            Allen Kaijage

           0655106767
            kaijagejr@gmail.com

                    
     Miaka ya 1950 alikuwepo dereva mmoja mmarekani aitwae Blake.Blake alikua ni dereva wa mabasi ya abiria.Siku moja jioni wakati akiendesha gari lake aligundua kuna abiria wapatao watatu ambao ni wamarekani weupe wamesimama wakati huo huo kuna wamarekani weusi wamekalia siti.Blake aliamua kusimamisha gari na kuwaamuru wale watu weusi kusimama na kuwapisha watu weupe wakae.Baadhi yao wakatii amri ya blake lakini kuna mdada mmoja jasiri aligoma kusimama kuwapisha watu weupe wakae.Mdada huyo alijulikana kwa jina la Rosa Parks. Rosa ni mmoja wa watu waliokua mstari wa mbele kupigania uhuru wa watu weusi pamoja na Martin Luther jr.Blake alimtahadharisha Rosa asipokubali kusimama atawapigia simu polisi wamkamate.Rosa bado aliendelea kuweka mgomo na hapo ndipo Blake akawapigia simu polisi na Polisi wakaja kumkamata Rosa kwa kosa la ukaidi.Mpaka leo watu weusi bado wanamkumbuka Rosa..

     Stori hii ya luther haitofautiani na stori ya Wacatalonia.Kule nchini Spain hakuna watu wabaguzi kama Wacatalonia.Wao wanapenda vya kwao tu.Ubaguzi wao unawapeleka mpaka kuwaza kujitenga na Spain na Catalonia iwe nchi huru.Katiaka kitongoji kimoja cha Catalonia kiitwacho Santpedor ndipo alipozaliwa Pep Guardiola.Pep Guardiola kama Wacatalonia wengine nae ni mbaguzi kweli kweli.Pep guardiola alipojiunga na Barcelona kitu cha kwanza alichofikiria ni nafasi za Wacatalonia ndani ya timu ya Barcelona.Pep kila akiwaangalia Henry,Etoo ,Yaya Toure na Deco wakiwa kwenye kikosi cha kwanza cha Barcelona alikua hajisikii vizuri.Ukiangalia Wachezaji hao wote hawajazaliwa Catalonia pia baadhi wana  asili ya ngozi nyeusi.Kitendo kile kilikua kinamuumiza sana Guardiola.Guardiola akatafuta kila mbinu kuhakikisha wachezaji hao hawakipigi Barcelona na nafasi zao zinachukuliwa na Wacatalonia.Henry kisa chake kilikua pedro,Etoo akapewa Borjan, Yaya Toure akategwa kwa Sergio Bousquet na Deco akanasa kwa Xavi.Guardiola alifanya maamuzi magumu kwa ajili ya kuinusuru Catalonia yake.Kitendo cha Guardiola kuanza kuwasugulisha benchi Henry,Etoo,Deco na Yaya Toure akitofautiani sana na kitendo cha Blake kuwaamuru watu weusi wasimame kuwapisha watu weupe wakae kwenye siti.Henry kwenye kiwango chake,Yaya kwenye ubora wake walikubali kuwapisha kirahisi Bosquet na Pedro wachukue nafasi zao.Watu wengi hawakumuelewa Pep.Ila mwisho wa siku Wacatalonia wenzake hawakumuangusha na kuifanya Barcelona ya Pep iliyojaa wazawa wengi kuwa Barcelona bora kuwai kutokea.Pia Pep mpaka leo atakumbukwa kwa kutoa wachezaji saba wa kikosi cha kwanza cha Spain kilichomfunga Uholanzi kwenye fainali ya Kombe la Dunia mwaka 2010.Kwa ufupi Pep ndie alichangia kwa kiasi kikubwa mafanikio ya timu ya taifa ya Spain katika kombe la Dunia mwaka 2010.


     Kila nikitafakari Dhambi ya Guardiola naona faida ndani yake.Guardiola amenifanya kuhisi kuna dhambi nyingine ni tamu kwa wanaoifanya.Nawaza tu jinsi gani Tanzania tutafanikiwa tukiwa na Roho kama ya Wacatalonia.Ukiangalia ligi yetu tumekuwa tukiwatukuza sana wachezaji wa kigeni.Si wachezaji tu pia tumekuwa walamba miguu ya makocha wa kigeni.Najiuliza kama Wacatalonia wasingeamua kumpa kibarua mtoto wa nyumbani pep kama Barcelona  na Spain wangetisha vile?.Hapa bado nafikiria ingekuaje kama Kenny Mwaisabula angekua kocha wa Yanga,Seleman Matola kocha wa simba na Kali Ongala angekua kocha wa Azam.Nahisi mwaisabula nafasi ya Jaja angekuwa anampanga Bahanuzi au Tegete,Nafasi ya Niyonzima angekua anacheza Dilunga,Pia angekua anampa sana nafasi Msuva na ngasa kuliko Coutinho.Vivo hivyo kwa Selaman Matola,Mtola asingemfikiria Okwi kuliko singano na Chanongo,Asingekua na haja ya kumpapatikia Kwizera wakati yupo mtoto wa nyumbani Jonas Mkude,Pia ingekua rahisi kwa Maguli kupata nafasi mbele ya Kiongera.

     Lakini Maximo na Phiri hawawezi kufikiria kama Mwaisabula na Matola wanavyofikiria.Maximo na Phiri hawana uchungu na Tanzania.Damu nzito kuliko maji bwana .Matola na Mwaisabula wana uchungu sana na Taifa lao.Wanaumia kama mimi wakiona Tanzania inavyoyumba kisoka.Lakini hata siku moja usitarajie Maximo na Phiri watakua na maumivu hayo.Maximo ataendelea kuwapa kipaumbele ndugu zake Jaja na Coutinho huku na sisi tukiendelea kuwashangalia huku tukiwa tumesahau kuwa vipaji vya Msuva ,Tegete na Bahanuzi vinaenda kuteketea.Phiri nae kama kawaida ataendelea kuwapa kipaumbele akina okwi,Kiongera,Kwizera na Tambwe,wakati huo huo Jonas Mkude,Singano na Chanongo wakiendelea kusugua benchi jambo linalohatarisha vipaji vyao.

    Wengi watakuja juu na kuniambia kama jaja anajua kuliko tegete kwanini asipangwe? Nami ntakuuliza je wewe ulikua unaamini kama Pedro ni bora kuliko Henry?,Xavi ni zaidi ya Deco?,Messi ni zaidi ya Ronaldinho?,Bosquet ni zaidi ya Yaya Toure?.Wote tulikua hatuamini lakini kocha mzawa Guardiola alituaminisha na wote tukaamini na kukubali.Pia mimi  bado naamini Jaja si lolote kwa Bahanuzi na Tegete,Jonas mkude ana ubora zaidi ya kwizera kama kocha tu akiwaamini,Tatizo lililopo ni ngumu makocha wa kigeni kuwaamini wachezaji wetu kuliko wachezaji kutoka nje ya nchi.

    Kwangu huu ni wakati sahihi kwa timu kubwa za Simba,Yanga,na Azam kujivika roho za Wacatalonia kwa  kuwaamini makocha wazawa Kama Wacatalonia walivyomuamini Pep Guardiola.Naamini ni makocha wazawa tu ndio wataliokoa soka letu kwa kulinda na kuendeleza vipaji vya wachezaji wetu.Wakina Matola,Mwaisabula na Kibaden ndio watakaoistiri Tanzania yetu kama Guardiola alivyofanya kwa Wacatalonia.

                                                               

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    1 comments:

    1. GUADIOLA ALIKUTA KIKOSI CHA FRANK RKAD,YEYE ALIFANYA MACHACHE TU GARI LIKAWAKA,NI DHAMBI KUMUANGUSHIA SIFA ZOTE YEYE WAKATI ALIKUTA MWENZIE KAMTENGENEZEA WATU ALIPOONA WANACHOKA AKAWAKIMBIA,KIPIMO CHAKE KIZURI NI BAYERN NGOJA TUONE ATAFIKA NAO WAPI MAANA LAST YR UKITOA BUNDESILIGA ALIVURUNDA CHAMPIONS LG NA KULE KWINGINE

      ReplyDelete

    Item Reviewed: DHAMBI YA GUARDIOLA DARASA KWA SOKA LA BONGO Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top