728x90 AdSpace

  • Latest News

    Sunday, September 21, 2014

    CHICHARITO:MANCHESTER HAWAKUNIAMINI KABISA MSIMU ULIOPITA



    Javier Hernandez Chicharito ameitupia dongo klabu yake mama ya Manchester United na kudai kuwa haikumuamini kabisa katika misimu miwili iliopita.


    Chicharito (26) raia wa Mexico ndani ya misimu miwili iliyopita alifanikiwa kuanza michezo isiyozidi kumi (10) kikosi cha kwanza akifanya mahojiano jana baada ya kuiwezesha klabu yake ya Real Madrid anayoichezea kwa mkopo kuibuka na ushindi mkubwa wa bao 8-2 dhidi ya klabu ya Derpotivo la Coruna alisema..


    “ Hakukuwa na imani.Ilinibidi kuwa na subira na ndiyo maana leo niko hapa.Msimu uliopita ulikuwa ni mgumu sana kwangu sababu sikuaminika.”

    Nilipata kukutana na {Carlo} Ancelotti wakati ule akiifundisha Chelsea.Imani aliyonayo kwa wachezaji wake imeniamsha na kunifanya nijitume zaidi”


    “Nataka kuutumia vizuri muda wangu wa kuwa hapa.Kila mchezaji anaota kuchezea Real Madrid.Najua niko hapa kwa sababu.Takwimu zinanibeba,mimi ni mchezaji mzuri nan i mtu wa watu”alimaliza Chicharito ambaye jana alianza kufungua akaunti yake ya magoli kwa kuifungia Real Madrid goli mbili baada ya kuingia kuchukua nafasi ya Gareth Bale.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: CHICHARITO:MANCHESTER HAWAKUNIAMINI KABISA MSIMU ULIOPITA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top