728x90 AdSpace

  • Latest News

    Sunday, September 21, 2014

    MILNER AKIENDEA DARASANI KIHISPANIA



    Habari na Paul Manjale

    Wakati kocha mkuu wa klabu ya Manchester United Mdachi Louis Van Gaal akiwataka wachezaji wake wote wanaongea kihispania kufanya kila wawezalo kujua kiingereza ili waweze kuendana vizuri na mazingira ya klabuni hapo kama mafunzo na mambo mengine hali ni tofauti kidogo kwa kiungo wa klabu ya Manchester City Muingereza James Milner.



    Milner ambaye ni mmoja kati ya wachezaji wachache wa kiingereza wanaopata nafasi ya kucheza kila juma klabuni hapo ameona kuwa dawa ya kurahisisha mawasiliano kati yake na wachezaji wenzake hasa wale wanaotoka Hispania na Amerika ya kusini ni kuamua kuiendea darasani lugha ya Kihispania.


    Hayo yamewekwa bayana na mlinzi wa zamani wa klabu hiyo aliyetimkia klabu ya Fiorentina (Fiola) ya Italia Micah Richards wakati akifanya mahojiano na jarida la The Guardian.Richards  amesema 
    Milner akiteta jambo mazoezini na David Silva hii ni mwaka 2011


    “Kwa miaka kadhaa sasa Milner amekuwa akijifunza Kispania ili aweze kuwasiliana na akina Aguero,David Silva,Pablo Zabaleta,Martin Demichelis,Ruben Cousilas na kocha Manuel Pellegrini.Nakumbuka kuna wakati nahodha Vincent Kompany aliwahi kuwaambia wachezaji wote wanaoongea Kihispania wajifunze Kiingereza lakini bado wamekuwa wazito kufanya hivyo”
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MILNER AKIENDEA DARASANI KIHISPANIA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top