728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, September 01, 2014

    KUTOKA LA LIGA:BARCA YAUA,MADRID YADUNDWA



    Paul Manjale
    0717 70 55 48

    Klabu ya Real Madrid iliyokuwa na nyota wao kibao wa bei mbaya imekubali kichapo cha goli 4-2 toka kwa klabu ya Real Sociedad katika mchezo mkali uliopigwa katika dimba la Anoeta.

    Madrid iliyokuwa bila ya nyota wake Cristiano Ronaldo ndiyo iliyokuwa ya kwanza kutikisa nyavu za wenyeji Sociedad baada ya kupata magoli ya haraka haraka kupitia kwa mlinzi Sergio Ramos na winga Gareth Bale.Baada ya magoli hayo Sociedad walikuja juu na kufanikiwa kurudisha goli moja baada ya jingine na kasha kuongeza kupitia washambuliaji wake hatari wakiongozwa na David Zuruzuta(41,65),Inigo Martinez (35) na Carlos Vela (75).


    Katika mchezo mwingine wa La Liga klabu ya Barcelona imeendeleza wimbi lake la ushindi baada ya kuifunga timu ngumu ya Villareal kwa goli 1-0 kupitia kwa kinda wake Sandro Ramirez (19) dakika ya 82 ya mchezo huo uliopigwa katika dimba la El Madrigal.


    Sandro akicheza mchezo wake wa kwanza akiwa na kikosi cha kwanza cha Barcelona aliingia dimbani kuchukua nafasi ya Pedro Rodriguez na kufanikiwa kufunga bao hilo muhimu na la pekee kufuatia kazi nzuri iliyofanywa na mchezaji bora wa zamani wa dunia Leonel Messi baada ya kuwazidi unjanja walinzi viburi wa Villareal.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: KUTOKA LA LIGA:BARCA YAUA,MADRID YADUNDWA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top